RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

CHEMSHA BONGO

MAAGIZO: Hurusiwi kuangalia jibu kabla ya kumaliza kujibu maswali Yote. Msimamizi wetu ni Yesu Kristo. Unapojibu tuonyeshe umejibu swali la ngapi, kwa mfano 1(a) au 3(c). Mungu akubariki Sana

SEHEMU YA 14

KITABU CHA YOHANA 7

MASWALI

1. Kwanini Yesu hakutaka kutembea katika eneo la Wayahudi na badala yake alitembea katika eneo la Galilaya?

2. Taja jina la sikukuu ya Wayahudi

3. Kwanini Yesu alisema, “Ulimwengu hauwezi kuwachukia nyinyi, bali kunichukia mimi” ?

4. Bwana Yesu alipoamua kukwea kwenda Galilaya kula sikukuu hata kama wakati wake wa kwenda haukutimia. Je, alikwea kwa uwazi au kwa siri?

5. Kwanini watu hawakuweza kumtaja Yesu katika ile sikukuu ya vibanda iliyoandaliwa kwa Wayahudi?

6. Yesu aliwambia kitu gani Wayahudi alipokuwa akifundisha baada ya Wayahudi kustaajabu na kujiuliza kuwa Yesu amepata wapi elimu?

7. Malizia mane haya ya Yesu, “Yeye aamiaye kwa nafsi yake tu hutafuta (i)……………………; bali yeye anayetafuta utukufu wake aliyempeleka yaani Mungu huyo ni kweli wala ndani yake hamna (ii)………………….

8. Kwanini Wayahudi walishindwa kumua Yesu alipokuwa akiwafundisha hekaluni?

9. Ni watu gani waliwatuma watumishi kwenda kumkamata Yesu?

10. Ni maneno gani Yesu alisema katika Roho siku ile ya mwisho wa sikukuu ya vibanda ya Wayahudi akiwa hekaluni?

MAJIBU


1. Wayahudi walitaka kumuua (Yohana 7:1)

2. Vibanda (Yohana 7:2)

3. Kwasababu Yesu alishuhudia kuwa kazi za dunia ni mbovu (Yohana 7:7)

4. Siri (Yohana 7:6)

5. Kwasababu ya kuwaogopa Wayahudi (Yohana :7….)

6. Mafunzo yangu si yangu ila ni Yake aliyenipeleka (Yohana 7:16)

7. (i) utukufu wake mwenyewe
(ii) Udhalimu

8. Kwasababu saa yake ilikuwa haijaja bado (Yohana 7:30)

9. Wakuu wa Makuhani na Mafarisayo (Yohana 7:32)

10. Mtu akiona kiu na aje kwangu anywe, aaminiye mimi kama vile maandiko yaliyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake (Yohana 7:37)

---------------------------------------------------------------------------------------

SEHEMU YA 13
KITABU CHA YOHANA 6
MASWALI

1. Kitu gani kiliwafanya makutano kumfuata Yesu alipokwenda zake ng’ambo ya Bahari ya Galilaya?

2. Yesu alipokwea mlimani, alikuwa na akina nani?

3. Pasaka ilikuwa ni siku ya akina nani?

4. Yesu alimwambia nani alipoona mkutano mkuu wanakuja pale alipoinua macho yake na kusema, “Tununue wapi mikate ili hawa wapate kula”?

5. Kwanini Yesu aliuliza swali hili kwa wanafunzi wake, “Tununue wapi mikate ili hawa wapate kula”?

6. Ni nani kati ya wanafunzi wa Yesu aliyeweza kuona mikate kutoka kwa motto aliyekuwa na mikate mitano na shayiri na samamki wawili?

7. Baada ya Yesu kuwaketisha watu wapatao elfu tano na kuwapa mikate na samaki na kwapa kadiri ya walivyotaka, nao waliposhiba walikusanya mabaki ya mikate na samaki vikapu vingapi?

8. Ni akina nani walisema, “Hakika huyu ni Nabii Yule ajae ulimwenguni?”

9. Yesu alichukua uamuzi gani baada ya kuona watu wamepanga kuja kumshika ili wamfanye mfalme?

10. Yesu alimaanisha nini aliposema, “Baba”?

11. Tufanyaje ili kuzitenda kazi za Mungu?

12. Malizia semi hizi za Yesu Kristo
(i) Amini amini nawaambieni………………………….
(ii) Wote anipao Baba watakuja kwangu, wala yeyote ajaye kwangu…………………..
(iii) Hakuna ajae kwangu (Yesu) isipokuwa amejariwa na…………………….

13. Tufanyaje ili tupate kuzitenda kazi za Mungu?

14. Chakula cha Mungu ni chakula cha namna gani?

15. (a) Yesu alishuka kutoka mbinguni ili afanye mapenzi kwa nani?
(b) Taja mapenzi ambayo Yesu alitumwa na Mungu kuyafanya hapa duniani?

16. Ni siku gani Yesu aliwaambia Wayahudi wasinung’unike juu ya Yeye kujiita ni chakula kilichoshuka kutoka mbinguni bali atawafufua na hakuna mtu ajae kwake asipovutwa kwa Baba aliyempeleka ulimwenguni?

17. Ni kitu gani anakipata Yule anayemwamini Mungu?

18. Yesu anasema yeye ni chakula cha uzima kilichoshuka kutoka wapi?

19. Ni hasara ganitunapata tusipokula mwili wa mwana wa Adam na kunywa damu yake?

20. Ni sehemu gani Yesu alisema maneno juu ya kula chakula chake ambacho kinatupa uzima wa milele na pia kunywa damu yake?

21. Ni chakula cha aina gani ambacho anasema tukila tutapata uzima wa milele?

MAJIBU

1. Kwasababu waliona ishara alizozifanyia wagonjwa (Yohana 6J1)

2. Wanafunzi (Yohana 6:3)

3. Wayahudi (Yohana 6:4)

4. Filipo (Yohana 6:5)

5. Kwasababu alitaka kuwajaribu kwa maana alijua mwenyewe atakalolitenda (Yohana 6:6)

6. Andrea nduguye Simoni Petro (Yohana 6:8)

7. Vikapu 12 (Yohana 6:13)

8. Ni wale watu waliona ishara alizofanya Yesu (Yohana 6:14)

9. Alienda mlimani Yeye peke yake (Yohana 6:15)

10. Mungu (Yohana 6:27)

11. Mwamini Yeye aliyetumwa na Yeye (Yohana 6:29)

12. (i) Sitamtupa kamwe (Yohana 6:37)
(ii)Baba yangu (Yohana 6:65)

13. Tumwamini Yeye aliyetumwa na Mungu (Yohana 6:29)

14. Chakula kitokacho mbinguni na kuwapa ulimwengu uzima (Yohana 6:30)

15. (a)Mapenzi Yake aliyempeleka (Yohana 6:38)
(b) Katika wote alionipa nisimpotezee hata mmoja bali nimfufue siku ya mwisho (Yohana 6:40)

16. Siku ya mwisho (Yohana 6:43)

17. Uzima wa milele (Yohana 6:47)

18. Mbinguni (Yohana 6:51)

19. Hakuna uzima ndani yetu, na hatafufuliwa siku ya mwisho (Yohana 6:54)

20. Katika Sinagogi huko Kaepernamu(Yohana 6:59)

21. Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu (Yohana 6:63)

---------------------------------------------------

SEHEMU YA 13
KITABU CHA YOHANA 5

1. Yesu alienda wapi siku ya sikukuu ya Wayahudi?

2. Bethazatha ni nini?

3. Watu gani waliokuwa wakingoja maji yachemke pale Yesu alipofika Yerusalem?

4. Watu gani walikuwa wakitibua maji katika birika linaloitwa Bethazatha?

5. Yesu alimwambia nani kuwa “Wataka kuwa mzima”?

6. Yesu alimwambia nini Yule mtu aliyekuwa hajiwezi kwa muda wa miaka 38 baada ya kuponywa na Yesu?

MAJIBU

1. Yerusalem (Yohana 5:1)

2. Birika iliyokuwa katika mlango wa kondoo (Yohana 5:2)

3. Viwete, waliopooza, vipofu (Yohana 5: 3)

4. Malaika (Yohana 5: 4)

5. Palikuwa na mtu ambaye alikuwa hajiwezi kwa muda wa miaka 38 (Yohana 5:5)

6. “Simama Jitwike godoro lako na uende” (Yohana 5:8)


-----------------------------------------------

SEHEMU YA 12
KITABU CHA YOHANA 4

MASWALI.

1. Yesu alipofika katika mji wa Samaria uitwao Sikari, karibu na shamba Yakobo alimpa Yusufu mwanae. Taja jina la kisima kilichokuwepo mahali hapo.

2. Yesu aliomba maji kwa nani baada ya kuchoka pale kwenye kisima cha Yokobo kutoka na safari yake kuwa ndefu, huku akisema, “Nipe maji ninywe”

3. Je, Wayahudi kipindi cha nyuma walikuwa wanachangamana na Wasamaria?

4. Maji ya Yesu ni maji ya namna gani?

5. Kitu gani kinaweza kumtokea mtu ambaye akinywa maji ya Yesu katika maisha yake?

6. Yesu alimwambia nini Yule mjane aliyemuomba maji ya uhai kutoka kwa Yesu?

7. Yule mjane aliyeambiwa na Yesu akamwite mume wake, alimjibu nini Yesu?

8. Malizia semi hii
(a) Nyinyi mnaabudu msichokijua, sisi tunaabudu…………………………..kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi
(b) Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabudio halisi………………………….
(c) Mungu ni……………., nao wamwabuduo yeye inawapasa kumwabudu katika……………………
(d) Nabii hapati heshima katika……………………………………..

9. Masihi ni na nani?

10. Taja eneo au mji amabo Yesu alifanya maji kuwa divai

MAJIBU

1. Yakobo (Yohana 4:6)

2. Msamalia (Yohana 4:7)

3. Hapana (Yohana 4:9)

4. Hai (Yohana 4:10)

5. Hatapata kiu milele (Yohana 4:14)

6. Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa (Yohana 4:16)

7. Sina mume (Yohana 8:17)

8. (a) Tukijuacho (Yohana 4:22)
(b) watamwabudu Baba katika Roho na kweli (Yohana 4:23)
(c) Roho, Roho na kweli (Yohana 4:24)
(b) nchi yake mwenyewe (Yohana 4:46)

9. Kristo (Yohana 4)

10. Kana ya Galilaya (Yohana 4:46)

----------------------------------------------------
SEHEMU YA 11
KITABU CHA YOHANA 3


MASWALI
  1. Taja jina la Mfarisayo mkuu wa Wayahudi aliyetaka kujua zaidi kuhusiana na ishara alizokuwa akifanya Yesu.
  2. Malizia usemi huu aliosema Yesu kwa Mkuu wa Wayahudi
    (a) "Amini, amini ninakuambia, mtu asipozaliwa mara ya pili,....................................................
    (b) Kilichozaliwa kwa mwili ni...............................na kilichozaliwa kwa Roho ni ....................
    (c) Lile tulijualo........................ na lile tulionalo....................................wala ushuhuda wetu hamwukubali.
    (d) Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala.......................matasadiki wapi niwaambiapo mambo ya......................?
  3. Nikodemo alipomuuliza Yesu akitaka kujua itakuwaje mtu kuzaliwa mara ya pili akiwa mzee? Yesu alimwambia nini?
  4. Biblia inasema wala hakuna aliyepaa mbinguni ila  aliyeshuka kutoka mbinguni. Taja jina la mtu aliyeshuka kutoka mbinguni?
  5. Kitu gani unaweza kupata ukimwamini Mwana wa Adamu?
  6. Malizia semi hizi:
    (a) Kwa  maana jinsi hii Mungu aliupenda........................na watu wakapenda...............
MAJIBU
  1. Nikodemo (Yohana 3:1)
  2. (a) hawezi kuona ufalme wa Mungu (Yohana 3:3)
    (b) mwili, Roho (Yohana 3: 6)
    (c) twalinena, twalishuhudia (Yohana 3:11)
    (d) hamkusadiki, mbinguni (Yohana 3:12)
  3. Amini, amini ninakuambia mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho hawezi kuingia ufalme wa Mungu (Yohana 3:5)
  4.  Mwana wa Adamu (Yohana 3:11)
  5. Uzima wa milele (Yohana 315)
  6. (a) ulimwengu
    -------------------------------------------------------------------------

SEHEMU YA 10
KITABU CHA YOHANA 2


MASWALI
  1. Taja mji ambao Yesu na wanafunzi wake pamoja  na mama yake walialikwa katika arusi?
  2. Mama yake Yesu alimuomba nini Yesu pale arusini afanyiwe baada ya kuona wenyeji wametindikiwa?
  3. Yesu alitumia nini kupata divai pale arusi katika mji wa Galilaya huko Kana?
  4. Mabalasi aliyotumia Yesu Kristo kupata Divai yalitumika kama nini kwa Wayahudi?
  5. Yesu aliwaambia wanafunzi wafanye nini kupata Divai kwa kutumia mabalasi, na wampelekee nani ayaonje?
  6. Mkuu wa meza alimwambia nini bwana arusi juu ya divai iliyogeuzwa Yesu kutoka mabalasi na kuwa divai?
  7. Siku ya Pasaka ilivyokaribia Yesu alikwea kuelekea wapi?
  8. Vitu gani Yesu aliviona alipokwea kuelekea Yerusalemu?
  9. Yesu aliwaambia nini wale waliokuwa wakifanya biashara katika hekalu?
  10. Yesu aliwaambia ni muda ngapi alitalijenga hekalu la Baba baada ya kulivunja?
  11. Wayahudi walimwambia Yesu ni kwa muda gani wanafikiri Yesu angelijenga hekalu baada ya kulibomo)
  12. Yesu alikuwa akimaanisha nini juu ya kulijenga hekalu la Baba baada ya kulibomoa?
  13. Kwanini Yesu hakujiaminisha kwa Wayahudi hasa kipindi kile cha pasaha na hakutaka kushuhudia habari za wanadamu?
MAJIBU
  1. Mji wa Galilaya huko Kana (Yohana 2:1)
  2. Divai(Yohana 2:3)
  3. Mabalasi sita ya mawe (Yohana 2: 6)
  4. Kutawadha kutokana na desturi ya Wayahudi (Yohana 2:6)
  5. Wajalize mabalasi maji, wampelekee mkuu wa meza ayaonje (Yohana 2:8-9)
  6. Kila mtu wa kwanza huandaa divai iliyo njema, hata watu wakishakunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu, Wewe umeweka divai njema hata sasa. (Yohana 2:10)
  7. Yerusalem (Yohana 2:13)
  8. Aliona pale hekaluni watu waliokuwa wakiuza ng'ombe na kondoo na njiwa na wengine kuvunja fedha za wenye kuvunja fedha. (Yohana 2:14-16)
  9. Yaondoeni haya msifanye nyumba ya Baba yangu nyumba ya biashara. (Yohana 2:16)
  10. Siku tatu (Yohana 2:19)
  11. Miaka 46 (Yohana 2:20)
  12. Alimaanisha hekalu la mwili wake (Yohana 2:21)
  13. Yesu aliwajua wote (Wayahudi) nia yao kwa maana Yeye mwenyewe alijua yaliyo ndani ya mwanadamu (Yohana 2:24)
------------------------------------------------------------------
SEHEMU YA 9
KITABU CHA YOHANA 1

MASWALI
  1. Malizia aya hii
    Hapo mwanzo kulikuwapo na Neno, naye Neno alikuwa (a) .............................Huyo (b)....................alikuwa kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa Huyo. Hata pasipo Yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulikuwamo c)...................................... ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang'aa d)................................., wala giza halikuweza.
  2. Ni nani aliyetumwa kutoka kwa Mungu, ambaye alikuja kwa ushuhuda ili aishuhudie ile nuru wote wapate kuamini kwa yeye. Huyo hakuwa na ile nuru balia alikuja ashuhudie ile nuru?
  3. Biblia inasema Neno alifanyika mwili akakaa kwetu, ili sisi tuweze kuona nini?
  4. Taja baadhi vitu alizoshuhudia kuvitamka Yohana juu ya kuja kwa Yesu Kristo, pale alipopaza sauti yake?
  5. Ni watu gani walitumwa kumuuliza Yohana kujua kama yeye ni Yesu Kristo, na walitumwa na nani?
  6. Yohana alipoulizwa na Makuhani na Walawi kuwa Yeye ni nani wakitaka kujua kama atajiita ni Yesu Kristo, aliwajibuje?
  7. Yohana aliwajibu wale Makuhani na Walawi kuwa yeye siye Kristo bali ni nani?
  8. Njia gani Yohana alitumia kubatiza watu?
  9. Yesu alibatiza kwa njia gani?
  10. Toa maana ya neno Rabi
  11. Taja majina mawili ya watu waliomsikia Yohana akiwataka kumfuata Yesu
MAJIBU
  1. a)  Mungu  b) Mwanzo c) Uzima d) gizani (Yohana 1:1-5)
  2. Yohana (Yohana 1:6)
  3. Utukufu kama wa Mwana pekee wa atoakaye kwa Baba (Yohana 1:14)
  4. i) Ajaye nyuma yangu (Yohana) amekuwa mbele yangu kwa maana alikuwa kabla yangu
     ii) Katika utimilifu wake sisi sote tulipokea neema juu ya neema
     iii) Hakuna mtu aliyemuona Mungu wakati wowote; Mungu mwana wa pekee aliye katika kifuacha Baba huyu ndiye aliyemfunua(Yohana 1:15-18)
  5. Waliotumwa ni Makuhani na Walawi, waliowatuma ni Wayahudi (Yohana 1:19)
  6. Mimi siye Kristo. Yohana 1:20
  7. Mimi ni sauti ya mtu aliye nyikani, Inyosheni njia ya Bwana! Kama vile alivyonena Nabii Isaya. (Yohana 1: 23
  8. Maji (Yohana 1:26)
  9. Roho Mtakatifu (Yohana 1:33)
  10. Mwalimu (Yohana 1:38)
  11. Andrea na Simoni Petro
    -----------------------------------------------------
SEHEMU YA NANE

 KITABU CHA LUKA 15-20

MASWALI
  1. Jambo gani lilitokea mpaka Yesu akasema, kutakuwa na furaha kwa wenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwaajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu
  2. Malizia habari ya tajiri na maskini
    a) Palikuwa na tajiri aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula siku zote kwa anasa. Na maskini mmoja jina lake..........................huwekwa mlangoni pake anavidonda vingi naye alitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule  b) Hata mbwa wakaja wakamlamba............................ c) Ikawa yule masikini alikufa akachukuliwa na ............................. d) mpaka kifuani kwa........................ Yule tajiri naye akafa, akazikwa. e) Basi kule.............................. akainua macho yake aalipokuwa katika mateso, f) akamwona............................kwa mbali na g)......................... kifuani mwake h) akalia akasema,.................................................
  3. Malizia sentensi hii .
    a) Makwazo hayana budi kuja ila ole wake................................................
    b) Jilindeni kama ndugu yako akikosa................................................
    c) Imewapasa kumuomba Mungu siku zote, wala....................................
  4. Ni watu gani walisema Bwana tuongezee imani? Yesu aliwaambia nini hawa watu juu ya kuongezewa imani?
  5. Watu wenye ukoma walimwambia nini Yesu walipomuona kwa mbali, na Yesu alisema nini kwa hao wenye ukoma?
  6. Yule aliyepona ukoma alifanya nini kumtukuza Mungu?
  7. Yesu alimwambia nini Msamaria aliyepona ukoma baada ya kumtukuza?
  8. Yesu aliwajibu nini Mafarisayo walipomuuliza juu ya siku ya kuja ufalme wa Mungu?
  9. a)Taja jina la  aliyetamani kumuona Yesu katika mji wa Yeriko na alikuwa mtoza ushuru.
    b) Kwanini alihangaika kumuona Yesu?
    c) Alifanya nini kumuona huyu Yesu, na kwanini alifanya hivyo?
MAJIBU
  1.  Baada ya Mafarisayo na waandishi kunung'unika wakisema, Mtu huyu huwakaribisha wenye dhambi tena hula nao. Na aliweza kutoa mfano wa kondoo aliyepotea (soma Luka 15:1-7)
  2. a) Lazaro b)vidonda c) malaika d) Ibrahimu e) kuzimu f) Ibrahimu g) Lazaro h)Ee Baba Ibrahimu nihurumie , umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, aburudishe ulimi wangu, kwasababu ninateswa katika moto huu
  3. a) mtu yule ambaye yaja kwasababu yake!
    b) mwonye, akitubu msamehe
    c) Msikate tamaa
  4. Mitume, Yesu alisema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali mngeuambia mkuyu huu ng'oka ukapandwe baharini, nao ungewatii.
  5. Ee Yesu Bwana mkubwa uturehemu, alipowaona akawambia, Enendeni mkajionyeshe kwa makuhani
  6. Alimtukuza Mungu kwa sauti, akaanguka kifudifudi miguuni pake akamshukuru naye alikuwa Msamaria
  7. Enenda zako imani yako imekuponya
  8. Ufalme wa Mungu hauji kwa kuchunguza, wala hawatasema tazama, upo huku au kule, kwa maana tazama ufalme wa Mungu uko ndani yenu
  9. a) Zakayo.
    b) Kwasabau alikuwa mfupi sana na alitamani kumuona Yesu ni wa namna gani
    c) Alipanda juu ya mkuyu apate kumona kwa kuwa atakuja kupita njia ile

    MWISHO
    -------------------------------------------------------

SEHEMU YA SABA
KITABU CHA LUKA 5 HADI 10
1. Zamani za Herode kulikuwa na Kuhani, alitwa nani?

2. Malaika alimtabiria Zakaria kuwa atazaa mtoto wa jinsia gani?

3. Taja jina la Malaika aliyemtabiria Zakaria?

4. Malaika alimwambia nini Zakaria kwa kutosadiki maneno yake juu ya kuzaliwa kwa Yohana?

5. Watu walimtambuaje Zakaria alivyotoka nje ya hekalu akiwa bubu?

6. Mwezi wa ngapi mailaka Gabriel alitumwa na Mungu kwenda Galilaya?

7. Taja jina la mwanawali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu jina lake Yusufu

8. Salamu aliyopewa Mariamu na Malaika Gabriel “Salamu uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe” ili maanisha nini?

9. Malaika alimpa sifa zipe kwa mtoto atakayezaliwa ambaye ni Yesu?

10. Kitu gani kilitokea kwa Elizabeth baada ya kuamkiwa na Mariamu?

11. Elizabeth alimzaa mtoto wa jinsia gani?

12. Kinywa cha Zackaria kilifunguliwa baada ya tukio gani na kuanza kunena na kumsifu Mungu?

13. Yesu alizaliwa katika mji gani?

14. Ishara gani waliambiwa wachungaji wataziona juu ya kuzaliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo?

15. Yesu alitahiriwa akiwa na umri gani?

16. Yesu alipelekwa wapi ili awekwe kwa Bwana?

17. Ni nani alionywa na Roho Mtakatifu kuwa hataona mauti kabla ya kumuona Kristo wa Bwana?

18. Yesu alibaki Yerusalemu akiwa na umri gani ambapo wazee wake hawakujua kuwa amebaki Yerusalemu?

19. Baada ya siku ngapi Yesu alipatikana hekaluni akiwa amekaa katikati ya walimu akiwasikiliza na kuwauliza maswali

20. Yesu alijibu nini kwa mama yake alipoulizwa, mwanangu mbona umetutenda hivi? Baada ya kumtafuta kwa muda wa siku tatu?

MAJIBU
  1.  Jibu: Kuhani –Zakaria, mke wake Elizabeth
  2. Jibu: Mwanaume ataitwa Yohana
  3. Jibu: Gabriel 
  4. Jibu: Atakuwa bubu 
  5. Jibu: Ameona maono ndani ya hekalu
  6. Jibu: Mwezi wa sita 
  7. Jibu: Mariamu 
  8. Jibu: Mariamu umepata neema kwa Mungu. Utachukua mimba na kumzaa motto jina lake utamwita Yesu. 
  9. Jibu: Atakuwa Mkuu, ataitwa mwana aliyejuu, Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi 
  10. Jibu: Kitoto kichanga kiliruka ndani ya tumbo lake Elizabeth, na akajazwa Roho Mtakatifu 
  11. Jibu: Mwanaume 
  12. Jibu: Baada ya Elizabeth kumzaa mtoto na kupewa jina la Yohana na kukataliwa kuitwa Zakaria jina baba yake 
  13. Jibu: mji wa Daudi 
  14. Jibu: Watamkuta mtoto mchanga, amevikwa nguo za kitoto, amelala katika holi la kulia ng’ombe. 
  15. Jibu: siku nne
  16. Jibu: Yerusalem 
  17. Jibu: Simeoni 
  18. Jibu: miaka 12
  19. Jibu: Siku 3 
  20. Jibu: Hamjui kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu? 

SEHEMU YA SITA
KITABU CHA LUKA
MASWALI

  1. (a) Yesu alitumia njia gani kumponya mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu wa miaka kumi na nne ambaye alikuwa hajiwezi kujinyoosha kabisa?

    (b) Kwanini mkuu wa sinagogi alimkasirikia Yesu kutokana na kitendo cha kumponya mwanamke mwenye pepo?

  2. Yesu alipokuwa akielekea Yerusalem alikutana na mtu mmoja aliyemuuliza, Je, Bwana watu wanaokolewa ni wachache? Yesu alimjibu nini huyo mtu?

  3. Kwanini Mafarisayo walimwambia Yesu aondoke mahali alipokuwa anahubiri Yerusalemu kwenda mahali pengine?

  4. Yesu anasemaje kuhusiana na mtu kukaa vitivya mbele unapokuwa umealikwa katika harusi?
MAJIBU
  1. (a) Yesu alimwita akamwambia, mama umefunguliwa katika udhaifu wako. Akaweka mikono yake juu yake naye akanyooka mara hiyo akamtukuza Mungu (Luka 13:12-13)

    (b) Kwasababu Yesu alimponya siku ya Sabato (Luka 13:14)

  2. Jitahidi kuingia katika mlango ulio mwembamba maana nawaambia mtu wengi wataka kuingia wasiweze. Wakati wenye nyumba atakaposimama nje na kubisha mlango, mkisema, Ee Bwana tufungulie, yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako, ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika nia zetu (Luka 13:22-30)

  3. Kwasababu Herode alitaka kumuua (Luka 13:31)

  4. Ukialikwa na mtu harusini, usiketi katika kiti cha mbele, isiwe kwamba amealikwa mtu mwenye kustahimili kuliko wewe akaja yule aliwaalika wewe nay eye na kukuambia mpishe huyu! Ndipo utakapoanza haya kushika mahali pa nyuma, Bali ukialikwa, nenda ukaketi mahali pa nyumailia jae yule aliyekualika, akwambie rafiki yangu njoo mbele ya wote walioketi pamoja na nawe kwa maana kila ajikwezae atalisdhiwa, naye ajiadhiye atakwezwa.

MWISHO
-----------------------------------------------------------------------------
SEHEMU YA TANO
KITABU CHA LUKA

MASWALI
  1. Ni faida gani unaweza kupata kwa kuonyesha upendo kwa adui yako?

  2. Kwanini Mungu anatukataza tusihukumu, tusilaumu, kutoachilia?

  3. Unafikiri ni nini kilimponyayule akida ambaye alikuwa anaumwa na yuko karibu ya kufa?

  4. (a) Ni neon gani Yesu alisema kwa mama mjane aliyefiwa na motto wake wa pekee ambaye alikuwa anaishi mji wa Naini?

    (b) Yesu alifanya nini kumponya yule motto wa mama majane?

    (c) Je, maiti iliinuka?

    (d) Watu walioona maiti ameinuka, walifanya nini?

  5. Yohana alipoita wawili kati ya wanafunzi wa Ysu na kuwatuma kwa Yesu akiuliza, wewe ndiye tumtazamiaye mwingine? Yesu aliwajibu nini wanafunzi?

  6. Kwanini wanasheria na Mafarisayo walipinga shauri la Mungu juu yao la kwamba, katika wale waliozaliwa na mwanamke hakuna aliye mkuu kuliko Yohana, lakini aliye mdogo katika ufamle wa Mungu ni mkuu kuliko yeye?

  7. (a) Kwanini mama yake na ndugu zake Yesu hawakuweza kumkaribia Yesu?

    (b) Yesu aliwambia nini wale waliomletea habari ya kwamba mama yake na ndugu zake wamesimamam nje wakataka kuonana naye?


  8. (a) Yesu alifanya nini pale chombo alichokuwa anasafiria Yeye na wanafunzi kilipoanza kuzama kutokana na tufaniiliyoshuka juu ya ziwa?

    (b) Baada ya msukosuko kukoma kutokana na maji, Yesu aliwambia nini wanafunzi wake?

  9. Yesu alipofika Pwani ya nchi ya Wagerasi inayoelekea Galilaya, alikutana na mtu mwenye pepo, hakuvaa nguo siku nyingi, wala hakukaa nyumbani, ila makaburini, alipofungwa minyororo na pingu alivikata na kukimbizwa jangwani kwa nguvu za yule pepo

    (a) Alipoulizwa na Yesu jina lake, alijibu nini?

    (b) Nini maaana ya jina hilo la huyo mwenye pepo?

    (c) Yesu aliwaamuru hao pepo waende wapi?

    (d) Baada ya pepo kwenda kule ambako Yesu aliwaamuru waende, ni kitu gani kilitokea kwa hao waliopokea hayo mapepo?

    (e) Yule aliyetolewa pepo alipoomba aongozane na Yesu, Je Yesu alisemaje?

  10. (a) Yesu aliposikia habari kuwa mtoto wa Mkuu wa sinagogi kuwa amekufa, ni kitu gani alikifanya?



MAJIBU
  1. Thawabu yetu itakuwa nyingi, na tutakuwa wana wa Aliye Juu kwa kuwa Yesu ni mwema kwa wasionishukuru na waovu (Luka 6:35)

  2. Tusihukumu nasi tutahukumiwa, tusilaumu nasi hatutalaumiwa, tuachilie nasi tutaachiliwa (Luka 6:37-38)

  3. Imani (Luka 7:2-10)

  4. (a) Usilie (luka 7:13)

    (b) aligusa jeneza na akasema, “Kijana nakwambia Inuka (Luka 7)

    (c) Ndiyo, yule maiti aliinuka na akaketi na kuanza kusema (Luka 7:15)

    (d) Hofu ikawashika wote wakamtukuza Mungu, wakisema, Nabii mkuu ametokea kwetu, na Mungu amewaangalia watu wake (Luka 7:16)

  5. Nendeni mkamweleze Yohana hayo yote mlioyaona na kuyasikia, vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea na wenye ukoma wanatakasika, maskini wanahubiriwa Habari Njema. Naye heri mtu yeyote asiyechukizwa nami (Luka 7:22-23)

  6. Kwasababu hawakubatizwa na Yohana, lakini watu wote na watoza ushuru waliposikia hayo, walikiri haki ya Mungu kwa kuwa wamebatizwa kwa ubatizo wa Yohana (Luka 7:28-30)

  7. (a) kwasababu ya mkutano (Luka 8:19)

    (b) Aliwajibu akasema, mama yangu na ndugu zangu ndio hao wasikiao Neno la Mungu na kulifanya (Luka 18:21)

  8. (a) Yesu aliamka akakemea upepo na msukosuko wa maji, vikakoma, kukawa shwari

    (b) Imani yenu iko wapi? (Luka 8:25)

  9. (a) Jeshi (Luka 8:30)

    (b) Pepo wengi wameniingia (Luka 8:30)

    (c) nguruwe (Luka 8:33)

    (d) Walitelemka gengeni kwa kasi, wakaingia ziwani, wakafa majini (Luka 8:33)

    (e) Akamwambia. “Rudi nyumbani kwako ukahubiri yaliyo makuu, Mungu aliyokutendea (Luka 8:39)

  10. (a) Yesu alimwambia Usiwe na hofu, amini tu na yeye ataponywa (Luka 8:50)
MWISHO
-------------------------------------------------------------------------------------------------


SEHEMU YA NNE
KITABU CHA LUKA
MASWALI
  1. (a) Yesu aliingia kwenye chombo cha nani cha kuvulia samaki wakati wavuvi wakiwa wametoka kuosha nyavu zao?

    (b) Je, Yesu alifundisha watu waliokuwa katika chombo cha wavuvi?

    (c) Ni kitu gani Simoni Petro alikifanya kwa Yesu baada ya kuona samaki aliokuwa anavua wamejaa katika vyombo vyao viwili?

    (d) Unafikiri Simoni Petro alishikwa na mshangao alipoona samaki ni wengi sana, yeye pamoja na Yakobo na Yohana?

    (e) Yesu aliwaambia nini, Simon baada ya kushangazwa na wingi wa samaki ambao hakutegemea kuwavua?

  2. (a) Mtu mwenye ukoma, alifanya nini ili alipomuona Yesu na aliomba nini kwa Yesu?

    (b) Yesu alifanyaje kumponya mtu mwenye ukoma?

    (c) Baada ya kutakasika mwenye ukoma, Yesu alimwambia nini cha kufanya kwa kuhani?

  3. (a) Baada ya watu waliomchukua mtu mwenye kupooza kukosa nafasi kutokana na wingi wa watu waliokuwa wakimsikiliza Yesu. Walitumia njia gani kumfikia Yesu ili amponye?

    (b) Yesu baada ya kuona imani ya waliombeba yule mwenye kupooza, aliwambia nini?

    (c) Waandishi walisema nini baada ya kuona Yesu ametoa msamaha wa dhambi kwa yule aliyepooza?

    (d) Yesu aliwaambia nini waadishi hao baada ya kuona mioyo yao?

    (e) Watu walipomuona yule mwenye kupooza akijitwika kile alichokilalia, Je, watu hao ni kitu gani walikifanya?

  4. (a) Taja jina la mtoza ushuru ambaye Yesu alikutana naye baada ya kumponya mwenye kupooza

    (b) Yesu aliambiwa nini na huyo mtoza ushuru baada ya kuonana naye?

    (c)  Kwanini Mafarisayo walinung’unika walipomuona Yesu anakula chakula na kunywa pamoja na watoza ushuru?

    (d) Karama ilifanywa na nani kuwakusanya mafarisayo, watoza ushuru na Yesu kula chakula na kunywa?

    (e) Yesu aliwajibuje wale Mafarisayo waliokuwa wanashangaa kuona Yesu anakula na watoza ushuru?

  5. Yesu alisema maneno haya baada ya kusikia nini kutoka kwa Mafarisayo, “Je, Mwaweza kuwafanya wafunge walioalikwa harusini, akiwapo Bwana harusi pamoja nao?” Lakini siku itakuja  watakapoondolewa Bwana harusi ndipo watakapofunga siku zile
MAJIBU
  1. (a) Simoni (Luka 5:3)

    (b) Ndiyo (Luka 5:4)

    (c) Alianguka magotini pa Yesu akisema, “Ondoka kwangu kwa maana mimi ni mwenye dhambi, Bwana” (Luka 5:8)

    (d)  Ndiyo walishikwa na mshangao (Luka 5:9)

    (e) “Usiogope, tangu sasa utakuwa ukivua watu” (Luka 5:10)

  2. (a) Alianguka kifudifudi na akamuomba Yesu akisema, “Baba ukitaka waweza kunitakasa” (Luka 5:12)

    (b) Aliunyosha mkono wake akamgusa akisema “Nataka takasika” (Luka 5:13)

    (c) Nenda ukajionyeshe kwa kuhani ukatoe kwaajili ya kutakasika kwako kama Musa alivyoamuru, iwe ushuhuda kwao” (Luka 5:14)

  3. (a) Walipanda juu ya dari wakampitisha katika matofali ya juu wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu (Luka 5:19)

    (b) Ee, rafiki umesamehewa dhambi zako (Luka 5:20)

    (c) Walihojiana wakisema, “Ni nani huyu asemaye maneno ya kukufuru? Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake? (Luka 5:21)

    (d) “Mnahojiana nini mioyoni mwenu? Kusema umesamehewa dhambi zako au kusema Ondoka, uende? Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi. (Luka 5:22-23)

    (e) Walishikwa na mshangao, wakamtukuza Mungu, wakajaa hofu, wakisema leo tumemuona mambo ya ajabu (Luka 5:25)

  4. (a) Lawi (Luka 5:27)

    (b) “Nifuate” (Luka 5:27)

    (c) Kwasababu watoza ushuru walionekana kuwa wenye dhambi (Luka 5:30)

    (d) Lawi (Luka 5:29)

    (e) Wenye afya hawana haja ya tabibu, isipokuwa walio hawawezi, sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi wapate kutubu (Luka 5:31)

  5.  Baada ya kuona wanafunzi kufunga mara nyingi, na kuomba dua, kadharika wanafunzi wa Mafarisayo, lakini wanafunza wa Yesu kunywa na kula (Luka 5:32)

---------------------------------------------------------------------------------------------------

SEHEMU YA PILI

KITABU CHA LUKA

MASWALI

  1. (a) Mwezi wa sita Mungu alimtumia Malaika Gabriel kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti kwa mwanamwali bikira aliyekuwa amepozwa na mtu, jina lake Yusufu, na huyo bikira jina lake Mariam. Malaika Gabriel alipoingia nyumbani kwake, alimwambia nini?

    (b)  Ni maneno gani malaika Gabriel alimjibu Elizabeti baada ya kuona amestajabishwa moyoni mwake baada ya kupokea salamu kutoka kwa malaika Gabriel ambayo hiyo salamu hakujua maana yake?

    (c) Ni kitu gani Malaika Gabriel  alimwimbia Elizabeti kuhusiana na mamlaka aliyokuwa nayo Yesu baada ya kuzaliwa kwake?

  2. Malaika alipomuuliza Malaika Gabriel yakuwa itakuwaje kuhusiana namimba wakati hamjui mume?

  3. (a) Kichanga cha Elizabeti mke wa kuhani Zakaria kilifanya nini tumboni mwa mama yake, baada ya Mariamu kusalimiana na Elizabeti?

    (b) Ni kitu gani kilimtokea Elizabetibaada ya kichanga kuruka ndani ya tumbo lake?

    (c) Mariamu alikaa na Elizabeti kwa muda gani kabla hajarudi nyumbani kwake?

  4. (a) Mtoto wa Elizabeti alitahiriwa siku ya ngapi?

    (b) Ni jina gani walitaka kumpa motto wa Elizabeti?

    (c) Elizabeti alikubaliana na jina la mwanae kuitwa zakaria? Kama hapana jina gani alimpa?

    (d) Je, watu walikubali motto wa Elizabeti kuitwa Yohana? Kama hapana
               (i) Kwanini walikataa?
               (ii) Walifanyeje kupata jina halisi?

    (e)  Nini kilimtokea Zakaria ambaye alikuwa haongei baada ya kuandika jina la motto wake katika kibao?

MAJIBU

  1. (a) Salamu uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe, Usiogope (Luka 1:28)

    (b)  Usiogope, Mariamu kwa maana umepata neema kwa Mungu, Tazama utachukua mimba na kuzaa mwanaume na jina lake utamwita Yesu (Luka 1:22)

    (c) Alimwambia
             (i) Yesu ataitwa mwana Aliye juu
             (ii) Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake
             (iii) Atamiliki nyumba ya Yakobohata milele
             (iv) Ufalme wake hatakuwa na mwisho
              (Luka1:32-33)

  2. Malaika akamwambia, Roho Mtakatifu atakuujia juu yako, na nguvu zake zitakufunika kama kivuli, kwasababu hicho kitakachozaliwa kitakuwa kitakatifu, Mwana wa Mungu (Lika 1:35)

  3. (a) Kitoto kichanga kiliruka ndani ya tumbo lake (Luka 1:41)

    (b) Elizabeti alijazwa na Roho Mtakatifu, akapaza sauti kwa nguvu, akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake wote, naye mzawa wa tumbo lako amebarikiwa (Luka 1:41-42)

    (c) Muda wa miezi mitatu (Luka 1:56)

4. (a) Siku ya nane (Luka 1:59)

(b) Jina la baba yake la Zakaria (Luka 1:60)

(c) Hapana, bali alimpa jina la Yohana (Luka 1:60)

(d) (i) Hawakukubali kuitwa Yohana kwasababu katika jamii yao hakuna mtu anaitwa hivyo

(ii) Wakamwashiria baba yake wajue atakavyomwita Zakaria akataka kibao na kuandika jina lake kuwa Yohana Luka 1:61-63)

(e) Kinywa chake kilifunguliwa na ulimi wake pia, akaanza kunena akisifu Mungu (Luka 1:64) na akajazwa na Roho Mtakatifu (Luka 1:67)


--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

SEHEMU YA KWANZA

KITABU CHA LUKA

Mtunzi: Rulea Sanga


MASWALI

  1. Taja jina la mke wa Kuhani Mkuu Zakaria, zamani za ufalme wa Herode.

  2. (a) Je, Kuhani Mkuu Zakaria na mkewe Elizabeti walikuwa nahaki mbele za Mungu?

    (b) Taja majina ya watoto wa kuhani mkuu zakaria, isipokuwa Yohana aliyempata uzee.

    (c) Kati ya kuhani mkuu Zakaria na mkewe Elizabeti, ni nani alikuwa tasa?

  3. (a) Kuhani Zakaria aliambiwa na nini na Malaika wa Bwana alipomuona ana hofu baada ya kumuona huyo malaika wakati akivukiza uvumba?

    (b) Kwanini Malaika wa Bwana alimwambia Kuhani Zakaria kuwa mkewe Elizabeti atamzaa Yohana naye Yohana atakuwa na furaha na shangwe na watu wengi watafurahia kuzaliwa kwake?

  4. Zakaria alijibiwa nini na Malaika alipomwambia Malaika, Nitajuaje Neno hilo? Maana ni mzeee, mke wangu ni mkongwe wa siku nyingi ?

  5. (a) Watu waliokuwa wanasubiri Kuhani Zakaria kutoka nje ya hekalu, walifanya nini walipoona anakawia kutoka hekaluni?

    (b) Zakaria alipotoka nje huku hawezi kuongea, watu walifikiria nini?

    (c) Mke wa kuhani Zakaria alitwaa mamba kipindi gani?

  6. (a) Mwezi wa sita Mungu alimtumia Malaika Gabriel kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti kwa mwanamwali bikira aliyekuwa amepozwa na mtu, jina lake Yusufu, n huyo bikira jina lake Mariam. Malaika Gabriel alipoingia nyumbani kwake, alimwambia nini?


MAJIBU

  1.  Elizabeti (Luka 1:5)

  2. (a) Walikuwa na haki mbele za Mungu (luka 1:6)

    (b) Hakuwa na mtoto (Lika 1:7)

    (c) Elizabeti Luka 1:7)

  3. (a) Alimwambia, Usiogope, kwa maana dua yako imesikiwa na mkeo Elizabetiatakuzalia motto mwanaume, utamwita Yohana (Luka 1:13)

    (b) kwasababu atakuwa Mkuu mbele za Bwana, hatakunywa divai, wala kileo, naye atajazwa Roho Mtakatifu (Luka 1:15)

  4. Malaika akajibu akamwambia, mimi ni Gabriel nisamamaye mbele za Mungu, nami nimetumwaniseme nawe na kukupasha habari hizo njema! Na tazama utakuwa bubu, usiweze kusema, mapak siku yatakapotukia hayo yatatimizwa kwa wakati wake (Luka 1:19)

  5. (a) Walisajabu (Luka 1:21)

    (b) Walitanbua kuwa ameona maono (Luka 1:22)

    (c) Siku za huduma za Kuhani Zakaria zilipotimia (Luka 1:23)


  6. (a) Salamu uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe, Usiogope (Luka 1:28)


MWISHO


---------------------------------------------------------------------------------------------------------

MTIHANI WA MWISHO WA MWEZI KUTOKA KATIKA KITABU CHA MARKO

MUDA WA KUFANYA MTIHANI: Masaa manne t

ONYO: Huruhusiwi kutumia Biblia au njia yoyote kupata majibu, tumia BONGO yako. Ukienda kinyume utakuwa unavunja taratibu za mtihani huu na moja kwa moja utakuwa umetenda DHAMBI. Kama jibu hulijua ni afadhali UKAACHA.

Tuma majibu yako kwa Barua Pepe rumatz2011@yahoo.com, Ruma Africa itasahihisha na kukupa cheti chako cha USHINDI.

SEHEMU YA KWANZA

Chagua najibu matano kicsha uyajibu.


MASWALI
  1. (i) Vazi alilovaa Yesu ulipokaribia wakati wa  kusulubiwa kwake lilikuwa la rangi gani?

    (ii)  Taja baadhi ya adhabu alizozipata Bwana Yesu kutoka kwa Wayahudi wakati ulipokaribia kusulubiwa?

    (iii) Ni nani alishurutishwa ili achukue msalaba wake?

  2. (i) Nini maana ya Golgotha?

    (ii) Mvinyo aliopewa Yesu ulitiwa nini?

  3. Yesu alisulubiwa saa ngapi pale mavazi yake yalivyopigiwa kura?

  4. Anwani ya mashitaka iliandikwaje juu ya msalaba?

  5. Wanyang’anyi wangapi walisulubishwa na Yesu?

  6. (i) Watu waliokuwa wakipita njiani na kumuona Yesu  amesulubiwa, walisema maneno gani?

    (ii) Wakuu wa makuhani nao walisema nini juu ya Yesu alipokuwa amesulubiwa?

  7. (i) Wakati Yesu amesulubishwa, ilipofika saa sita, kulitokea nini?

    (ii) Ilipofika saa tisa, Yesu alipaza sauti gani?

    (iii) Watu waliosimama mahali pale ambapo Yesu akipaza sauti walisema nini na kile Yesu alikisema?

  8. Ni akina nani walionunua manukato ili wapate kwenda kumpaka Yesu siku ya sabato baada ya Yesu kushushwa msalabani na kuviringishwa jiwe mbele ya mlango wa kaburi?

  9. (i) Mariamu Magadalene, Mariamu mamaye Yakobo, na Salome walipoingia ndani ya kaburi la Yesu ili wampake manukato waliona nini?

    (ii) Ni maneno gani huyo kijan aliyekuwa kaburini aliwambia, Mariamu Magadalene, na Mariamu mamaye Yakobo, na Salome walipoingia kaburini mwa Yesu ili wampake manukato Yesu?

SEHEMU YA PILI
Chagua maswali matatu, lakini swali la kwanza ni lazima kulijibu

MASWALI

  1. (i) Kwanini Petro alisema  “ Rabi, ni vizuri sisi kuwepo hapa; na tufanye vibanda vitatu, kimoja chako wewe, kimoja cha Musa, kimoja cha Eliya?

    (ii) Ni sauti gani ilitoka baada ya wingu kutokea na kuwatia vuli Petro Yakobo na Yohana walipokuwa mlimani wakati Yesu akigeuka sura na mavazi yake kung’ara na kuwa meupe mno?

    (iii) Baada ya kusikia hiyo sauti, waliona nini?


  2. (i)Yesu alimwambia nini yule mtu aliyemleta mwanae mwenye pepo bubu ambalo humwaga chini na kusababisha kutoa povu na kusaga meno na kudondoka kutona na wanafunzi wa Yesu kushindwa kumtoa yule pepo?

    (ii)  Yesu alipowaambia wamlete  yule mwenye pepo kuja kwake, pepo lilimfanyeje huyo mwenye pepo?

    (iii)  Yesu alivyomuuliza baba yake na yule mwenye pepo kuwa ni lini alipatwa na pepo, na nini kilikuwa kikimtokea, alijibiwa nini?

    (iv) Baada ya Yesu kujibiwa, huyo mwenye motto mwenye pepo alimuomba Yesu afanye nini juu ya mgonjwa wake?

    (v) Ni maneno gani Yesu alimwambie yule baba wa mototo mwenye pepo lililomfanya bubu, baada ya kuambiwa amhurumie na kumsaidia?

    (vi) Ni kitu gani kilimtokea yule mwenye pepo bubu baada ya Yesu kukemea lile pepo?

    (v) Baada ya pepo kutolewa, Yesu aliwajibu nini wanafunzi wake walipomuuliza, kwanini wao hawakuweza kumtoa huyo pepo bubu?


  3. (i) Yesu alipoulizwa na Mafarisayo kuhusian na mume kumuacha mke wake kwa kumuandikia talaka, je, Yesu alitoa jibu gani?

    (ii) Yesu aliwambia nini wanafunzi wake kuhusiana na wale wanawaacha wake zao na kuoa wengine?


  4. (i) Baada ya wanafunzi kutaza watoto wadogo kumgusa Yesu, Yesu aliwaambia nini hao wanafunzi kuhusiana na watoto wadogo?

    (ii) Yesu aliwaonya nini hao wanafunzi kuhusiana na kuwakataza watoto wadogo wasimguse?

    (iii) Yesu alifanya nini kwa hao watoto wadogo baada ya kuwaonya wanafunzi wake waliokuwa wanawakatza watoto hao wasimguse Yesu?


  5. (i) Yesu alijibu nini yule mtu aliyemkimbilia na kupiga magoti mbele zake hasa pale aliposema “Mwalimu Mwema” wakati akitaka kujua ni jinsi gani afanye kurithi ufalme wa Mungu?

    (ii) Ni kitu gani Yesu alimwambia afanye  yule mtu aliyepiga magoti mbele za Yesu ili aweze kurithi ufalme wa Mungu hata kama hajawahi  hakuzini, hakuua, hakuiba, hakuhusudia uongo, hakudanganya, aliwaheshimu baba na mama yake tangia utoto wake?


SEHEMU YA TATU
Jibu maswali yote kwa usahihi
MASWALI
  1. (i) Mafarisayo wanavyosema mikono najisi, ni mikono ya aina gani? Maneno hayo walisema walipoona wanafunzi wa Yesu wakila chakula

    (ii) Mapokeo ya kutawaza kabla ya kula chakula waliipata wapi?

    (iii) Yesu aliwajibu nini baada ya kuulizwa sawli na Mafarisayo, “Mbona wanafunzi wako hawendi kw kufuata mapokeo ya wazee, bali hula chakula kwa mikono najisi?”

    (iv) Nini maana ya mfano wa unajisi aliutoa Yesu kwa wanafunzi wake walipomuuliza ili wapate kuelewa?
  1. (i) Yesu alipokuwa Tiro na  Sidonia, mwanamke alimwangukia miguuni pale, unafikiri ni kwanini alifanya hivyo?

    (ii) Huyu mwanamke alikuwa ni wa kabila gani?

    (iii) Je, huyo binti mwenye mapepo machafu alipona, na kama alipona ni baada ya Yesu kufanya nini?
(i) Yesu alifanye kumponya yule aliyekuwa kiziwi na ,wenye utasi alipokuwa nje ya mipaka ya Tiro?

(ii) Baada ya kupona huyo kiziwi na mwenye utasi, Yesu alimwambiaje kuhusu ushuhuda wake kwa watu?

SEHEMU YA NNE
Jibu matatu ila swali la tano na la nne ni lazima kulijibu

MASWALI
1.      (i) Yesu aliwahurumia makutano kwa kutokula chakula kwa muda wa siku tatu tangia amekuwa nao. Kwanini Yesu aliogopa kuwaaga bila ya kuwapa chakula?

(ii) Wanafunzi wa Yesu waliopomjibu Yesu kwa kuuliza swali, Je! Atawaweza wapi mtu kuwashibisha hawa mikate nyikani?, Je, Yesu aliwajibuje?

(iii) Yesu alifanya nini baada ya Yesu kujibiwa kuwa wanayo mikate saba na visamaki vichache?

(iii) Je, wanafunzi walishiba hiyo mikate saba na visamaki vichache?

(iv) Watu wangapi walikula hiyo mikate saba na visamaki vichache?


2.      Mafarisayo walipokuwa  wakihojiana na kutafuta ishara itokayo mbinguni, Yesu alisema nini juu ya hilo jaribu? 

3.      (i) Kwanini Yesu alisema maneno haya “ Je, mioyo yenu ni mizito? Mna macho hamuoni, mna masikio hamsikii? Wala hamkumbuki?”


4.      (i) Yesu alifanya ishara gani alipomponya yule kipofu Bethasaida?

(ii) Yule Kipofu alipoulizwa Je, Waona? Alimjibu nini Yesu?

(iii) Yesu alipojibiwa lile swala la Je, Waona?, nini alikifanya tena kwa huyo kipofu?


5.      Yesu alienda na nani mlimani ambako aligeuka sura yake, mavazi yake yakawa meupe mno yakameta-meta?

SEHEMU YA TANO
Chagua swali moja tu na ulijibu
MASWALI
  1. (i) Ni katika mazingira gani na aliona nini pale Yesu alisema maneno haya, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake mwenyewe, na kwa jamii zake, na nyumbani kwake.”

    (ii) Je, Yesu alifanya muujiza wowote baada ya kusema “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake mwenyewe, na kwa jamii zake, na nyumbani kwake.”


  2. (i) Ni vitu gani Yesu aliwakatasa wale Thenashara aliowatuma wawili wawili baada ya kuwapa amri juu ya pepo wachafu?

    (ii) Hao Thenashara walihubiri juu ya nini na vitu gani walivifanya kwa wale waliokuwa wanahubiriwa? 

SEHEMU YA SITA

MASWALI
  1. (i) Kwanini watu walimshangaa sana Yesu alipokuwa anafundisha siku ya sabato  katika sinagogi ya Kapernaumu.

    (ii) Ni mtu wa namna gani aliyepasa sauti akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je umekuja kutuangamiza?”

    (iii) Baada ya huyo mtu kusema maneno hayo hapo juu (swali la (ii)), Yesu alisemaje kwa huyo mtu?


  2. Taja miujiza ambayo Yesu aliwahi kuifanya katika kitabu cha Marko.


  3. Malizia misemo ifuatayo aliyosema Yesu:-

    (i) Dhambi zote watasamehewa wanadamu, na kufuru zao watakazokufuru zote, Bali mtu atakayekufuru Roho Mtakatifu…………………………….

    (ii) Kipimo kile mpimacho…………………………………………………

    (iii) Mwenye kitu atapewa na asiye na kitu………………………………..

    (iv) Ni kama punje ya haradani, ambayo ipandwapo katika nchi, ingawa ni ndogo kuliko mbegu zote zilizo katika nchi, ………………………………
****************************************************
 
MAJIBU YA SEHEMU YA KWANZA

1.      (i) Rangi ya zambarau (Marko 15:16)

(ii) Wayahudu walimfanyia Yesu yafuatayo:-

            (a) walimvika vazi la zambarau.

            (b) wakasokota taji la miiba, wakamtia kichwani.

            (c) Wakamsalimu “Salamu mfalme wa Wayahudi”

            (d) Wakampiga mwanzi kichwani
           
            (e) Wakamtemea mate

            (f)  Baada ya kuddhihakiwa walimvua lile vazi la zambarau, wakamvika
                  mavazi yake mwenyewe.

           (g) Wakamchukua nje ili wamsulubishe.

(iii) Simoni ndiye alishurutishwa wakati akitoka shambani ili abebe msalaba wake (Marko 15:21)

2.      (i) Golgotha maana yake Fuvu la kichwa (Marko 15:22)

(ii) Walimpa mvinyo iliyotiwa manemane, na hakuipokea (Marko 15:23)

3.      Ilikuwa saa tatu (Marko 15:25)

4.      Iliandkwa MFALME WA WA WAYAHUDI (Marko 15:26)

5.      Walikuwa wanyang’anyi wawili, mmoja mkono wake wa kuume na mmoja mkono wake wa kushoto. (Marko 15:27)

6.      (i) Nao waliokuwa wakipita njiani wakamtukana, wakatikisatikisa vichwa, wakisema, Ahaa! Wewe mwenyekuvunja hekalu na kulijenga siku tatu, jiponye nafsi yako, ushuke msalabani. (Marko 15:30)

(ii) Wakuu wa makuhani wakadhihaki wao kwa wao, pamoja na waandishi, wakisema, hawezi kujiponya mwenyewe. Kristo, mfalme wa Israel, na ashuke sasa msalabani tupate kuona na kuamini. (Marko 15:31-32)

7.      (i) Ilipokuwa saa sita, palikuwa na giza juu ya nchi yot. Marko 15:33)

(ii) Yesu alipaza sauti yake kwa nguvu, Eloi, Eloi lama sabakithani? Maana yake Mungu wangu mbona umeniacha? (Marko 15:34)

(iii) Walisema, Tazama anamwita Eliya. (Marko 15:35-37

8.      Mariamu Magadalene, na Mariamu mamaye Yakobo, na Salome. (Marko 15:1)



(i) Waliona kijana ameketi upande wa kuume, amevaa vazi jeupe, wakastajabu. (Marko 16:5)

(ii) Aliwambiwa, Msistaajabu, mnatafuta Yesu Mnazareti, aliyesulubiwa amefufuka, hayupo hapa, patazamenimahli walipomuweka. (Marko 16:6)

MWISHO
---------------------------------------------------------------------------------------------

MAJIBU SEHEMU YA PILI

  1. (ii) Kwasababu walikuwa na hofu na hawakujua la kunena kutoka na vile kutokana na Yesu kugeuka sura mbele yao, mavazi yake yakamete-meta na kuwa meupe mno jinsi asivyoweza dobi duniani kuyafanya meupe. Haya yalitokea pale mlimani ambapo Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana faraghani. (Marko 9:2-6)

    (ii) “Huyu ni mwanangu mpendwa msikilizeni yeye” (Marko 9:7)

    (iii) walimwona Yesu pekee yake. (Marko 9:8)

  2. (i)Yesu aliwajibu, akasema, “Enyi kizazi kisichoaamini, nikae nanyi hata lini, nichukuliane nanyi hata lini?”  (Marko 9:19)

    (ii)  Yule pepo alimtia kifafa, naye akaanguka chini, akagaagaa, akitokwa na povu. (Marko 9:20)

    (iii) Yesu alijibiwa kuwa alipatwa tangia alivyokuwa motto, na mara nyingi ametupwa katika moto, katika maji, amwangamize. (Marko 9:21)

    (iv) Alimwomba Yesu aseme neon lolote na amhurumie na kumsaidia. (Marko 9:22)

    (v) Yesu alimwambia akisema, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye. (Marko 9:23)

    (vi) Huyo mwenye pepo akalia, akamtia kifafa sana, akamtoka na yeye akawa kama amekufa (Marko 9:26)

    (v) Yesu akawaambia “ Namna hii hiwezi kutoka kwa neon lolote, isipokuwa kwa kuomba. (Marko 9:29)

  3. (i) Yesu aliwambia, Kwasababu ya ugumu wa mioyo yenu, Musa aliwandikia amri hii. Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mke na mume. Kwasababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye  ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja, hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe. (Marko 10:8-9)

    (ii) Yesu aliwaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na na kuoa mwingine azini juu yake, na mke akimwacha mumewe na kuolewa na mwingine , azini. (Marko 10:11)

  4. (i)  Yesu alichukizwa sana, na alimwaambia wanafunzi wake, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie kwa maana, watoto kama hawa ufalme wa Mugu ni wao. (Marko 10:14)

    (ii) Yesu akawambia, Amini na wambieni, Yeyote asiyekubali ufalme wa Mungu kama motto mdogo hatauingia kabisa. (Marko 10:15)

    (iii) Yesu akawabariki hao watoto. (Marko 10:16)

  5. (i) Yesu akasema, kwanini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja ndiye Mungu. (Marko 10:18)

    (ii) Yesu alimwambia, “Enenda ukauze ulivyonavyo vyote, uape maskini nawe utakuwa na hazina mbinguni, kasha njoo unifuate. (Marko 10:21)
MWISHO
-------------------------------------------------------------------------------------------------


MAJIBU SEHEMU YA TATU
  1. (i) mikono isiyonawiwa mpaka kiwiko na mikono isiyotawazwa kama wakitokea sokoni (Marko7:2)

    (ii) walipata kutoka kwa wazee wao (Marko 7:3)

    (iii) Aliwaambia, Isaka alitabiri vema juu  yenu ninyi wanafiki, kama ilivyoandikwa, Watu hawa hunieshimu kwa midomo, ila mioyo iko mbali nami, nao huniabudu bure, wakifundisha yaliyo ya wanadamu. Nanyi mwaiacha amri ya Mungu na  kuyashika mapokeo ya wanadamu. (Soma Marko 7:6-13)

    (iv)  Yesu alitoa maana yake kwa kusema, “Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi”,  kwa maana ndani ya mioyo ya watoto hutoa mawazo mabaya, uasherati, wivu, uuaji, uzinzi, tama mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu. Haya yote yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi u (Marko7:20-23)

  2. (i) alitaka binti yake mwenye mapepo machafu aliyekuwa nyumbani kwake apone (Marko 7:25)

    (ii) Ni Myunani kabila la Msirofoinike (Marko 7: 26)

    (iii) Alipona (Marko 7:30) baada ya kuona imani ya yule mwanamke na pale alipoambiwa na  Yesu ya kuwa “Waache watoto washibe  kwanza; kwa maana si vizuri kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa” na yule mwanamke akamjibu Yesu kwa kusema, “Naam, bwana lakini hata mbwa waliochini ya meza hula makombo ya watoto” Yesu akasema kwasababu ya neon hilo enenda zako, pepo amemtoka binti yako (Marko 7:27-30)

  3. (i) Yesu akatia vidole vyake masikioni mwake, akatema mate,  akamgusa ulimi, akatazama juu mbinguni, akaugua, akamwambia, Efatha, maana yake Funguka. Masikio yake yakafunguka na kifungo cha ulimi wake kikalegea, akasema vizuri  (Marko 7:33-36)

    (ii) Akawaonya wasimwambie mtu (Marko 736)

MWISHO
------------------------------------------------------------------------------------------------

MAJIBU SEHEMU YA NNE
1.      (i) Kwasbabu aliona watazimia njiani ni baadhi yao walitoka mbali. (Marko 8:1)

(ii)  Yesu aliwauliza, Mnayo mikate mingapi? (Marko 8:5)

(iii)  Yesu aliwaagiza mkutano waketi chini; akaitwaa ile mikate saba, akashukuru, akaimega, akawapa wanafunzi wakewawaandikie, wakaawandikia mkutano. Akavibariki visamaki vile vichache, akasema wawaandikie nahivyo pia. (Marko 8:6-7)

(iii) Ndiyo, walikula wakashiba wakakusanya mabaki ya vipande vya mikate makanda saba. (Marko 8: 8)

(iv) Watu waliokula yapata elfu nne. (Mako8:9)


2.      Aliwambia, “Mbona kizazi hiki chatafuta isahara? Amini nawambia, Hakitapewa ishara kizazi hiki” (Marko 8:12)


3.      Kwasababu wanafunzi wake walikuwa na wasiwasi kutokana na kutokuwa na mikate ya kutosha baada ya kusahau kuibeba na walikuwa na mkate mmoja tu katika chombo chao. (Marko 14)


4.      (i) Yesu akamshika mkono na akamtemea mate ya macho, akamuwekea mikono yake . (Marko 8: 23)

(ii) Alimjibu, Naona watu kama miti inakwenda. (Marko 8:24)

(iii) Yesu aliweka tena mikono yake juu ya macho yake, naye akatazama sana, akawa mzima, akaona vyote waziwazi. Marko 8:25)


5.      Yesu alienda na Petro, Yakobo na Yohana.(Marko 9:2)

MWISHO

MAJIBU  SEHEMU YA TANO
  1. (i) Maneno haya aliyasema siku ya sabato ambapo wengi walimshangaa akifundisha siku hiyo ya sabato katika sinagogi. Walisema, “Huyu ameyapata wapi?, na ni hekima gani hii aliyopewa huyu?, Na nini miujiza hii mikubwa inayotendeka kwa mikono yake?, Huyu sio seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo na Yose na Yuda na Simoni? Na Maumbo yake hayapo hapa petu. (Marko 6:1-6)

    (ii) Hakuweza kufanya muujiza wowote bali aliwaponya wagonjwa wachache kwa kuwawekea mikono juu. (Marko 6:5)



  2. (i) Aliwakataza yafuatayo:

    (a) Wasichukue kitu cha njiani isipokuwa fimbo tu; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni. Bali wajifungie viatu; akasema msivae kanzu mbili.

    (b) Mahali popote mtakapoingia katika nyumba kaeni humo hata mtakapotoka mahali pale.

    (c) Na mahali popote wasipowakaribisha ninyi wala kuwasikia mtokapo huko yakung’uteni mavumbi yaliyochini ya miguu yenu
    (Marko 6:10-11)

    (ii) walihubiri watu watubu. Wakatoa pepo wengi, wakapaka mafutawatu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza (Marko 612-13) 
MWISHO

MAJIBU SEHEMU YA SITA
  1. (i) kwasababu alikuwa anafundisha kama mtu mwenye amri wala si kama wandishi.(Marko 1:22)

    (ii) ni mtu mwenye pepo mchafu.(Marko 1:23)

    (iii)  Yesu akamkemea akisema, Fumba kinywa, na umtoke. (Marko 1: 25)


  2. Miujiza

    (i) Alimtakasa mtu mwenye

    (ii) Aliwaponya wenye pepo (Marko 1:32)

    (iii) Alimtakasa mtu mwenye ukoma (Marko 1:40)

    (iv) Alimsamehe dhambi mtu aliyepooza na kumponya (Marko 2:3)
(i) hana msamaha hata milele (Marko 3:28)

(ii) ndicho mtakachopimiwa, na tena mtazidishiwa (Marko 4:24)

(iii) hata kile alichonacho atanyang’anywa (Mrko 4:25)

(iv) lakini ikishakupandwa hukuwa, ikawa kubwa kuliko miti, yote ya mboga, ikifanya matawi makubwa, hata ndege wa angani waweza kukaa chini ya uvuli wake (Marko 4:31)


MWISHO
---------------------------------------------------------------------------------------------------------------
SEHEMU YA SITA KITABU CHA MARKO

MASWALI
  1. (i) Vazi alilovaa Yesu ulipokaribia wakati wa  kusulubiwa kwake lilikuwa la rangi gani?

    (ii)  Taja baadhi ya adhabu alizozipata Bwana Yesu kutoka kwa Wayahudi wakati ulipokaribia kusulubiwa?

    (iii) Ni nani alishurutishwa ili achukue msalaba wake?

  2. (i) Nini maana ya Golgotha?

    (ii) Mvinyo aliopewa Yesu ulitiwa nini?

  3. Yesu alisulubiwa saa ngapi pale mavazi yake yalivyopigiwa kura?

  4. Anwani ya mashitaka iliandikwaje juu ya msalaba?

  5. Wanyang’anyi wangapi walisulubishwa na Yesu?

  6. (i) Watu waliokuwa wakipita njiani na kumuona Yesu  amesulubiwa, walisema maneno gani?

    (ii) Wakuu wa makuhani nao walisema nini juu ya Yesu alipokuwa amesulubiwa?

  7. (i) Wakati Yesu amesulubishwa, ilipofika saa sita, kulitokea nini?

    (ii) Ilipofika saa tisa, Yesu alipaza sauti gani?

    (iii) Watu waliosimama mahali pale ambapo Yesu akipaza sauti walisema nini na kile Yesu alikisema?

  8. Ni akina nani walionunua manukato ili wapate kwenda kumpaka Yesu siku ya sabato baada ya Yesu kushushwa msalabani na kuviringishwa jiwe mbele ya mlango wa kaburi?

  9. (i) Mariamu Magadalene, Mariamu mamaye Yakobo, na Salome walipoingia ndani ya kaburi la Yesu ili wampake manukato waliona nini?

    (ii) Ni maneno gani huyo kijan aliyekuwa kaburini aliwambia, Mariamu Magadalene, na Mariamu mamaye Yakobo, na Salome walipoingia kaburini mwa Yesu ili wampake manukato Yesu?

MAJIBU

1.      (i) Rangi ya zambarau (Marko 15:16)

(ii) Wayahudu walimfanyia Yesu yafuatayo:-

            (a) walimvika vazi la zambarau.

            (b) wakasokota taji la miiba, wakamtia kichwani.

            (c) Wakamsalimu “Salamu mfalme wa Wayahudi”

            (d) Wakampiga mwanzi kichwani
           
            (e) Wakamtemea mate

            (f)  Baada ya kuddhihakiwa walimvua lile vazi la zambarau, wakamvika
                  mavazi yake mwenyewe.

           (g) Wakamchukua nje ili wamsulubishe.

(iii) Simoni ndiye alishurutishwa wakati akitoka shambani ili abebe msalaba wake (Marko 15:21)

2.      (i) Golgotha maana yake Fuvu la kichwa (Marko 15:22)

(ii) Walimpa mvinyo iliyotiwa manemane, na hakuipokea (Marko 15:23)

3.      Ilikuwa saa tatu (Marko 15:25)

4.      Iliandkwa MFALME WA WA WAYAHUDI (Marko 15:26)

5.      Walikuwa wanyang’anyi wawili, mmoja mkono wake wa kuume na mmoja mkono wake wa kushoto. (Marko 15:27)

6.      (i) Nao waliokuwa wakipita njiani wakamtukana, wakatikisatikisa vichwa, wakisema, Ahaa! Wewe mwenyekuvunja hekalu na kulijenga siku tatu, jiponye nafsi yako, ushuke msalabani. (Marko 15:30)

(ii) Wakuu wa makuhani wakadhihaki wao kwa wao, pamoja na waandishi, wakisema, hawezi kujiponya mwenyewe. Kristo, mfalme wa Israel, na ashuke sasa msalabani tupate kuona na kuamini. (Marko 15:31-32)

7.      (i) Ilipokuwa saa sita, palikuwa na giza juu ya nchi yot. Marko 15:33)

(ii) Yesu alipaza sauti yake kwa nguvu, Eloi, Eloi lama sabakithani? Maana yake Mungu wangu mbona umeniacha? (Marko 15:34)

(iii) Walisema, Tazama anamwita Eliya. (Marko 15:35-37)

8.      Mariamu Magadalene, na Mariamu mamaye Yakobo, na Salome. (Marko 15:1)

(i) Waliona kijana ameketi upande wa kuume, amevaa vazi jeupe, wakastajabu. (Marko 16:5)

(ii) Aliwambiwa, Msistaajabu, mnatafuta Yesu Mnazareti, aliyesulubiwa amefufuka, hayupo hapa, patazamenimahli walipomuweka. (Marko 16:6)

MWISHO-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

SEHEMU YA TANO KITABU CHA MARKO
MASWALI
  1. (i) Kwanini Petro alisema  “ Rabi, ni vizuri sisi kuwepo hapa; na tufanye vibanda vitatu, kimoja chako wewe, kimoja cha Musa, kimoja cha Eliya?

    (ii) Ni sauti gani ilitoka baada ya wingu kutokea na kuwatia vuli Petro Yakobo na Yohana walipokuwa mlimani wakati Yesu akigeuka sura na mavazi yake kung’ara na kuwa meupe mno?

    (iii) Baada ya kusikia hiyo sauti, waliona nini?

  2. (i)Yesu alimwambia nini yule mtu aliyemleta mwanae mwenye pepo bubu ambalo humwaga chini na kusababisha kutoa povu na kusaga meno na kudondoka kutona na wanafunzi wa Yesu kushindwa kumtoa yule pepo?

    (ii)  Yesu alipowaambia wamlete  yule mwenye pepo kuja kwake, pepo lilimfanyeje huyo mwenye pepo?

    (iii)  Yesu alivyomuuliza baba yake na yule mwenye pepo kuwa ni lini alipatwa na pepo, na nini kilikuwa kikimtokea, alijibiwa nini?

    (iv) Baada ya Yesu kujibiwa, huyo mwenye motto mwenye pepo alimuomba Yesu afanye nini juu ya mgonjwa wake?

    (v) Ni maneno gani Yesu alimwambie yule baba wa mototo mwenye pepo lililomfanya bubu, baada ya kuambiwa amhurumie na kumsaidia?

    (vi) Ni kitu gani kilimtokea yule mwenye pepo bubu baada ya Yesu kukemea lile pepo?

    (v) Baada ya pepo kutolewa, Yesu aliwajibu nini wanafunzi wake walipomuuliza, kwanini wao hawakuweza kumtoa huyo pepo bubu?

  3. (i) Yesu alipoulizwa na Mafarisayo kuhusian na mume kumuacha mke wake kwa kumuandikia talaka, je, Yesu alitoa jibu gani?

    (ii) Yesu aliwambia nini wanafunzi wake kuhusiana na wale wanawaacha wake zao na kuoa wengine?

  4. (i) Baada ya wanafunzi kutaza watoto wadogo kumgusa Yesu, Yesu aliwaambia nini hao wanafunzi kuhusiana na watoto wadogo?

    (ii) Yesu aliwaonya nini hao wanafunzi kuhusiana na kuwakataza watoto wadogo wasimguse?

    (iii) Yesu alifanya nini kwa hao watoto wadogo baada ya kuwaonya wanafunzi wake waliokuwa wanawakatza watoto hao wasimguse Yesu?

  5. (i) Yesu alijibu nini yule mtu aliyemkimbilia na kupiga magoti mbele zake hasa pale aliposema “Mwalimu Mwema” wakati akitaka kujua ni jinsi gani afanye kurithi ufalme wa Mungu?

    (ii) Ni kitu gani Yesu alimwambia afanye  yule mtu aliyepiga magoti mbele za Yesu ili aweze kurithi ufalme wa Mungu hata kama hajawahi  hakuzini, hakuua, hakuiba, hakuhusudia uongo, hakudanganya, aliwaheshimu baba na mama yake tangia utoto wake?

MAJIBU
  1. (ii) Kwasababu walikuwa na hofu na hawakujua la kunena kutoka na vile kutokana na Yesu kugeuka sura mbele yao, mavazi yake yakamete-meta na kuwa meupe mno jinsi asivyoweza dobi duniani kuyafanya meupe. Haya yalitokea pale mlimani ambapo Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana faraghani. (Marko 9:2-6)

    (ii) “Huyu ni mwanangu mpendwa msikilizeni yeye” (Marko 9:7)

    (iii) walimwona Yesu pekee yake. (Marko 9:8)

  2. (i)Yesu aliwajibu, akasema, “Enyi kizazi kisichoaamini, nikae nanyi hata lini, nichukuliane nanyi hata lini?”  (Marko 9:19)

    (ii)  Yule pepo alimtia kifafa, naye akaanguka chini, akagaagaa, akitokwa na povu. (Marko 9:20)

    (iii) Yesu alijibiwa kuwa alipatwa tangia alivyokuwa motto, na mara nyingi ametupwa katika moto, katika maji, amwangamize. (Marko 9:21)

    (iv) Alimwomba Yesu aseme neon lolote na amhurumie na kumsaidia. (Marko 9:22)

    (v) Yesu alimwambia akisema, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye. (Marko 9:23)

    (vi) Huyo mwenye pepo akalia, akamtia kifafa sana, akamtoka na yeye akawa kama amekufa (Marko 9:26)

    (v) Yesu akawaambia “ Namna hii hiwezi kutoka kwa neon lolote, isipokuwa kwa kuomba. (Marko 9:29)

  3. (i) Yesu aliwambia, Kwasababu ya ugumu wa mioyo yenu, Musa aliwandikia amri hii. Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mke na mume. Kwasababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye  ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja, hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe. (Marko 10:8-9)

    (ii) Yesu aliwaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na na kuoa mwingine azini juu yake, na mke akimwacha mumewe na kuolewa na mwingine , azini. (Marko 10:11)

  4. (i)  Yesu alichukizwa sana, na alimwaambia wanafunzi wake, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie kwa maana, watoto kama hawa ufalme wa Mugu ni wao. (Marko 10:14)

    (ii) Yesu akawambia, Amini na wambieni, Yeyote asiyekubali ufalme wa Mungu kama motto mdogo hatauingia kabisa. (Marko 10:15)

    (iii) Yesu akawabariki hao watoto. (Marko 10:16)

  5. (i) Yesu akasema, kwanini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja ndiye Mungu. (Marko 10:18)

    (ii) Yesu alimwambia, “Enenda ukauze ulivyonavyo vyote, uape maskini nawe utakuwa na hazina mbinguni, kasha njoo unifuate. (Marko 10:21)


MWISHO

-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------


SEHEMU YA NNE KITABU CHA MARKO

MASWALI
  1. (i) Mafarisayo wanavyosema mikono najisi, ni mikono ya aina gani? Maneno hayo walisema walipoona wanafunzi wa Yesu wakila chakula

    (ii) Mapokeo ya kutawaza kabla ya kula chakula waliipata wapi?

    (iii) Yesu aliwajibu nini baada ya kuulizwa sawli na Mafarisayo, “Mbona wanafunzi wako hawendi kw kufuata mapokeo ya wazee, bali hula chakula kwa mikono najisi?”

    (iv) Nini maana ya mfano wa unajisi aliutoa Yesu kwa wanafunzi wake walipomuuliza ili wapate kuelewa?
  1. (i) Yesu alipokuwa Tiro na  Sidonia, mwanamke alimwangukia miguuni pale, unafikiri ni kwanini alifanya hivyo?

    (ii) Huyu mwanamke alikuwa ni wa kabila gani?

    (iii) Je, huyo binti mwenye mapepo machafu alipona, na kama alipona ni baada ya Yesu kufanya nini?
  1. (i) Yesu alifanye kumponya yule aliyekuwa kiziwi na ,wenye utasi alipokuwa nje ya mipaka ya Tiro?

    (ii) Baada ya kupona huyo kiziwi na mwenye utasi, Yesu alimwambiaje kuhusu ushuhuda wake kwa watu?

MAJIBU
  1. (i) mikono isiyonawiwa mpaka kiwiko na mikono isiyotawazwa kama wakitokea sokoni (Marko7:2)

    (ii) walipata kutoka kwa wazee wao (Marko 7:3)

    (iii) Aliwaambia, Isaka alitabiri vema juu  yenu ninyi wanafiki, kama ilivyoandikwa, Watu hawa hunieshimu kwa midomo, ila mioyo iko mbali nami, nao huniabudu bure, wakifundisha yaliyo ya wanadamu. Nanyi mwaiacha amri ya Mungu na  kuyashika mapokeo ya wanadamu. (Soma Marko 7:6-13)

    (iv)  Yesu alitoa maana yake kwa kusema, “Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi”,  kwa maana ndani ya mioyo ya watoto hutoa mawazo mabaya, uasherati, wivu, uuaji, uzinzi, tama mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu. Haya yote yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi u (Marko7:20-23)

  2. (i) alitaka binti yake mwenye mapepo machafu aliyekuwa nyumbani kwake apone (Marko 7:25)

    (ii) Ni Myunani kabila la Msirofoinike (Marko 7: 26)

    (iii) Alipona (Marko 7:30) baada ya kuona imani ya yule mwanamke na pale alipoambiwa na  Yesu ya kuwa “Waache watoto washibe  kwanza; kwa maana si vizuri kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa” na yule mwanamke akamjibu Yesu kwa kusema, “Naam, bwana lakini hata mbwa waliochini ya meza hula makombo ya watoto” Yesu akasema kwasababu ya neon hilo enenda zako, pepo amemtoka binti yako (Marko 7:27-30)

  3. (i) Yesu akatia vidole vyake masikioni mwake, akatema mate,  akamgusa ulimi, akatazama juu mbinguni, akaugua, akamwambia, Efatha, maana yake Funguka. Masikio yake yakafunguka na kifungo cha ulimi wake kikalegea, akasema vizuri  (Marko 7:33-36)

    (ii) Akawaonya wasimwambie mtu (Marko 736)

MWISHO
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Mwandishi: Rulea Sanga


SEHEMU YA TATU KITABU CHA MARKO

MASWALI

1.      (i) Yesu aliwahurumia makutano kwa kutokula chakula kwa muda wa siku tatu tangia amekuwa nao. Kwanini Yesu aliogopa kuwaaga bila ya kuwapa chakula?

(ii) Wanafunzi wa Yesu waliopomjibu Yesu kwa kuuliza swali, Je! Atawaweza wapi mtu kuwashibisha hawa mikate nyikani?, Je, Yesu aliwajibuje?

(iii) Yesu alifanya nini baada ya Yesu kujibiwa kuwa wanayo mikate saba na visamaki vichache?

(iii) Je, wanafunzi walishiba hiyo mikate saba na visamaki vichache?

(iv) Watu wangapi walikula hiyo mikate saba na visamaki vichache?

2.      Mafarisayo walipokuwa  wakihojiana na kutafuta ishara itokayo mbinguni, Yesu alisema nini juu ya hilo jaribu? 

3.      (i) Kwanini Yesu alisema maneno haya “ Je, mioyo yenu ni mizito? Mna macho hamuoni, mna masikio hamsikii? Wala hamkumbuki?”

4.      (i) Yesu alifanya ishara gani alipomponya yule kipofu Bethasaida?

(ii) Yule Kipofu alipoulizwa Je, Waona? Alimjibu nini Yesu?

(iii) Yesu alipojibiwa lile swala la Je, Waona?, nini alikifanya tena kwa huyo kipofu?

5.      Yesu alienda na nani mlimani ambako aligeuka sura yake, mavazi yake yakawa meupe mno yakameta-meta?

MAJIBU
1.      (i) Kwasbabu aliona watazimia njiani ni baadhi yao walitoka mbali. (Marko 8:1)

(ii)  Yesu aliwauliza, Mnayo mikate mingapi? (Marko 8:5)

(iii)  Yesu aliwaagiza mkutano waketi chini; akaitwaa ile mikate saba, akashukuru, akaimega, akawapa wanafunzi wakewawaandikie, wakaawandikia mkutano. Akavibariki visamaki vile vichache, akasema wawaandikie nahivyo pia. (Marko 8:6-7)

(iii) Ndiyo, walikula wakashiba wakakusanya mabaki ya vipande vya mikate makanda saba. (Marko 8: 8)

(iv) Watu waliokula yapata elfu nne. (Mako8:9)

2.      Aliwambia, “Mbona kizazi hiki chatafuta isahara? Amini nawambia, Hakitapewa ishara kizazi hiki” (Marko 8:12)

3.      Kwasababu wanafunzi wake walikuwa na wasiwasi kutokana na kutokuwa na mikate ya kutosha baada ya kusahau kuibeba na walikuwa na mkate mmoja tu katika chombo chao. (Marko 14)

4.      (i) Yesu akamshika mkono na akamtemea mate ya macho, akamuwekea mikono yake . (Marko 8: 23)

(ii) Alimjibu, Naona watu kama miti inakwenda. (Marko 8:24)

(iii) Yesu aliweka tena mikono yake juu ya macho yake, naye akatazama sana, akawa mzima, akaona vyote waziwazi. Marko 8:25)

5.      Yesu alienda na Petro, Yakobo na Yohana.(Marko 9:2)

MWISHO
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------


SEHEMU YA PILI KUTOKA KITABU CHA MARKO


MASWALI
  1. (i) Ni katika mazingira gani na aliona nini pale Yesu alisema maneno haya, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake mwenyewe, na kwa jamii zake, na nyumbani kwake.”

    (ii) Je, Yesu alifanya muujiza wowote baada ya kusema “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake mwenyewe, na kwa jamii zake, na nyumbani kwake.”

  2. (i) Ni vitu gani Yesu aliwakatasa wale Thenashara aliowatuma wawili wawili baada ya kuwapa amri juu ya pepo wachafu?

    (ii) Hao Thenashara walihubiri juu ya nini na vitu gani walivifanya kwa wale waliokuwa wanahubiriwa?
     

MAJIBU
  1. (i) Maneno haya aliyasema siku ya sabato ambapo wengi walimshangaa akifundisha siku hiyo ya sabato katika sinagogi. Walisema, “Huyu ameyapata wapi?, na ni hekima gani hii aliyopewa huyu?, Na nini miujiza hii mikubwa inayotendeka kwa mikono yake?, Huyu sio seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo na Yose na Yuda na Simoni? Na Maumbo yake hayapo hapa petu. (Marko 6:1-6)

    (ii) Hakuweza kufanya muujiza wowote bali aliwaponya wagonjwa wachache kwa kuwawekea mikono juu. (Marko 6:5)


  2. (i) Aliwakataza yafuatayo:

    (a) Wasichukue kitu cha njiani isipokuwa fimbo tu; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni. Bali wajifungie viatu; akasema msivae kanzu mbili.

    (b) Mahali popote mtakapoingia katika nyumba kaeni humo hata mtakapotoka mahali pale.

    (c) Na mahali popote wasipowakaribisha ninyi wala kuwasikia mtokapo huko yakung’uteni mavumbi yaliyochini ya miguu yenu
    (Marko 6:10-11)

    (ii) walihubiri watu watubu. Wakatoa pepo wengi, wakapaka mafutawatu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza (Marko 612-13) 
MWISHO
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

SEHEMU YA KWANZA KUTOKA KITABU CHA MARKO

MASWALI
  1. (i) Kwanini watu walimshangaa sana Yesu alipokuwa anafundisha siku ya sabato  katika sinagogi ya Kapernaumu.

    (ii) Ni mtu wa namna gani aliyepasa sauti akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je umekuja kutuangamiza?”

    (iii) Baada ya huyo mtu kusema maneno hayo hapo juu (swali la (ii)), Yesu alisemaje kwa huyo mtu?

  2. Taja miujiza ambayo Yesu aliwahi kuifanya katika kitabu cha Marko.

  3. Malizia misemo ifuatayo aliyosema Yesu:-

    (i) Dhambi zote watasamehewa wanadamu, na kufuru zao watakazokufuru zote, Bali mtu atakayekufuru Roho Mtakatifu…………………………….

    (ii) Kipimo kile mpimacho…………………………………………………

    (iii) Mwenye kitu atapewa na asiye na kitu………………………………..

    (iv) Ni kama punje ya haradani, ambayo ipandwapo katika nchi, ingawa ni ndogo kuliko mbegu zote zilizo katika nchi, ………………………………

MAJIBU
  1. (i) kwasababu alikuwa anafundisha kama mtu mwenye amri wala si kama wandishi.(Marko 1:22)

    (ii) ni mtu mwenye pepo mchafu.(Marko 1:23)

    (iii)  Yesu akamkemea akisema, Fumba kinywa, na umtoke. (Marko 1: 25)

  2. Miujiza

    (i) Alimtakasa mtu mwenye

    (ii) Aliwaponya wenye pepo (Marko 1:32)

    (iii) Alimtakasa mtu mwenye ukoma (Marko 1:40)

    (iv) Alimsamehe dhambi mtu aliyepooza na kumponya (Marko 2:3)

  3. (i) hana msamaha hata milele (Marko 3:28)

    (ii) ndicho mtakachopimiwa, na tena mtazidishiwa (Marko 4:24)

    (iii) hata kile alichonacho atanyang’anywa (Mrko 4:25)

    (iv) lakini ikishakupandwa hukuwa, ikawa kubwa kuliko miti, yote ya mboga, ikifanya matawi makubwa, hata ndege wa angani waweza kukaa chini ya uvuli wake (Marko 4:31)
MWISHO
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

MITIHANI WA MWISHO WA MWEZI JULAI 2012 WA CHEMSHA BONGO NA BIBLE
Unatakiwa kujibu maswali yote kwa muda wa saa mbili na nusu. Tunaamini utazingatia hilo agizo kwasababu wewe ni mtumishi wa Mungu.

Majibu yako unaweza kunitumia katika email yangu rumatz2012@yahoo.com.

Angalia muda ulioanza kujibu kwa makini.

Kumbuka hapo ulipo unasimamiwa na Roho Mtakatifu kwahiyo huwezi kufanya jambo lakuangalizia.

Ukiangalizia Roho Mtakatifu na nguvu za Mungu zitakutoa katika chumba chako cha kufanyia mtihani.

Matokeo yako utatumiawa kwa email na utapewa na cheti cha kufanya mtihani.

Kila swali lina maksi 10

Jinsi ya kujibu: Unatakiwa kuchagua jibu sahihi na ukipata andika namba ya jibu na jibu lake kwa kuandika herufi kama ni A, B, au C. Na usiandike swali, wewe tutumie hiyo herufu na namba ya swali.


MASWALI YOTE NI YA KUCHAGUA

Chagua jibu sahihi;

  1. Kitu gani kilitokea wakati Yesu anabatizwa

                 (a) Wingu jeusi

                  (b) Tetemeko la ardhi

                  (c) Mbingu za dunia zikamfunukia akaona Roho wa Mungu akishuka             
                 kama hua, akija juu yake, na sauti kutoka juu ikisema, Huyu ni
                 mwanagu mpendwa wangu, ninayependezwa naye

  2. Yesu alipopandishwa na Roho nyikani ili ajaribiwe na ibilisi, alifunga kula siku ngapi?

                  (a) kumi

                  (b) Sita

                  (c) Arobaini
  3.   (i) Yesu alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia, akimsihi akisema, Bwana mtumishi wangu amelala, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana. Yesu akamwambia,

                  (a) Amini ameshapona

                  (b) Nitakuja, nimponye

                  (c) Nitakuja, nimuokoe na atapona.

    (ii) Yule akijibu akasema, Bwana mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu, lakini sema neno na mtumishi wangu atapona. Yesu aliposikia hayo alistajabu akawambia wale waliomfuata

                  (a) Amini na wambie sijaona imani kubwa kama hii kwa yeyote
                 katika Israel

                  (b) Amini na wambie sijaona imani kubwa kama hii kwa yeyote
                 katika mkutano huu

                  (c) Amini na wambie sijaona upendo kubwa kama huu kwa yeyote
                 katika Israel

  4. (i) Kuna muujiza ambao Yesu aliufanya wa kuiongeza mikate na samaki ambapo wanafunzi wake walikula mpaka wakasaza. Ni mikate mingapi na samaki ngapi ambazo Yesu aliziombea kwa kutazama juu mbinguni kwa Mungu?

                  (a) Mikate miwili na samaki watano

                  (b) Samaki wawili na mikate mitano

                  (c) Mkate mmoja na samaki waili

    (ii) Masazo yaliyobaki baada ya wanafunzi kula na kushiba ilijaa vikapu vingapi?

                  (a) kumi na viwili

                  (b) Kuma na saba

                  (d) viwili

  5. Ni baada ya kufanya nini, Yesu aliwaambia, “Imeandikwa, nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala, bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi”.

                  (a) Ni baada ya Yesu kuingia hekaluni na kuona watu wakiuza na
                 kununua, Yesu akapindua meza za wabadili fedha na viti vyao
                 waliokuwa wanauzia njiwa

                  (b) Ni baada ya Yesu kuingia msikitini na kuona watu wakiuza na
                 kununua, Yesu akapindua meza za wabadili fedha na viti vyao
                 waliokuwa wanauzia njiwa

                  (c) Ni kabla ya Yesu kuingia hekaluni na kuona watu wakiuza na
                 kununua, Yesu akapindua meza za wabadili fedha na viti vyao
                 waliokuwa wanauzia njiwa
  6. (i) Yuda alipoona ya kuwa Ysu amekwisha kuhukumiwa, alifanya nini?

                  (a) Yuda alijuta akawarudishia wakuu na makuhani na wazee vile
                 vipande thelathini na moja vya fedha

                  (b) Yuda alijuta akawarudishia wakuu na makuhani na wazee vile
                 vipande thelathini vya fedha

                  (c) Yuda alijuta akawarudishia wakuu na makuhani na wazee vile
                 vipande thelathini vya dhahabu

    (ii) Ni maneno gani Yuda alisema baada ya kurudisha vile vipande alivyopewa kwaajili ya kumsaliti Yesu?

                  (a) Alisema, Nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia
                  (b) Alisema, Sijakosea nilipoisaliti damu isiyo na hatia
                  (c) Alisema, Nalikosa nilipoisaliti damu iliyo na hatia

    (ii) Yuda baada ya kukimbia ndani ya hekalu kutokana na kumsaliti Yesu alifanya nini?

                  (a) Alikimbia na kujinyonga

                  (b) Alirudi na kumsujudia Yesu

                  (c) Alihuzunika sana na kulia

  7. Baada ya kusikia kuwa Herode amekufa Misri, Yusufu, Yesu na Bikira Maria  walitoka Israel ni wapi walienda kuishi?

                  (a) Nazareti

                  (b) Misri

                  (c) Marekani
  8. Taja majaribu matatu ambayo Yesu alijaribiwa na Ibilisi nyikani?

                  (a) (i) Mawe yawe mikate

                      (ii) Yesu kujitupa chini kutoka katika kinara cha hekalu

                      (iii) Kumsujudia Ibilisi

                  (b) (i) Mchanga uwe mikate

                      (ii) Yesu kujitupa chini kutoka katika kinara cha mlima

                      (iii) Kumsujudia Ibilisi

                  (c) (i) Mawe yawe mikate

                      (ii) Yesu kujitupa chini kutoka katika kinara cha hekalu

                      (iii) Kumsujudia Mfalme
  9. Yesu aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata. Na tazama akaja mtu mwenye ukoma, akamsujudia akisema,

                  (a) Bwana ukitaka unaweza kunitakasa

                  (b) Bwana ukitaka waweza kunibariki

                  (c) Bwana ukitaka waweza kunihurumia

  10. (i) Taja jina la mfalme aliyemfunga na kumtia Yohana Mbatizaji gereza?

                  (a) Kayafa

                  (b) Rulea Sanga

                  (c) Mfalme Herode

    (ii) Kwani Yohana alifungwa gerezani?

                  (a)  Yohana alimwambia sio halali kwa Herode kuwa na nduguye   
                 Filipo awe mke wake na Herode.

                  (b) Yohana alimwambia sio halali kwa Kayafa kuwa na nduguye
                 Musa awe mke wake na Herode.

                  (c) Majibu ya hapo juu sio sahihi

    (iii) Kwanini mfalme alipoona watu akaogopa kumuua Yohana Mbatizaji?

                  (a)  Yohana alimwambia sio halali kwa Herode kuwa na nduguye
                 Filipo awe mke wake na Herode.

                  (b) Kwasababu watu walimuona Yohana Mbatizaji kama Nabii

                  (c) Kwasababu watu walimuona Yohana Mbatizaji kama Mfalme

    (iv) Ni nani aliyecheza mbele ya Herode wakati wa sikuku yake ya kuzaliwa akampendeza Herode kwa uchezaji wake?

                  (a) Binti Herode

                  (b) Mjukuu wa Herode

                  (c) Rafiki yake na Binti Herode

    (v) Ni nani alimshauri huyu mtu aliyecheza mbele ya mfalme Herode na mpaka Herode akakubali kutimiza kiapo chake cha kumpa chochote atakachoomba?

                  (a) mama yake

                  (b) Kaka yake

                  (c) Rafiki yake

    (vi) Huyo aliyemfurahisha Herode kwa kucheza aliomba  nini apewe na huyo mfalme?

                  (a) hakuomba chochote

                  (b) aliomba kichwa cha Yohana Mbatizaji katika mfuko

                  (c) aliomba kichwa cha Yohana Mbatizaji katika kombe

    (vii) Unafikiri Herode alifuarahia ilo ombi la huyu aliyecheza vizuri katika sikuku yake ya kuzaliwa? Na kama alifurahi au alisikitika ni kwanini?

                  (a) Herode alisikitika, kwasababu aliona ni aibu kwa watu waliokuwa
                 nao katika meza ya chakula na wote waliofika katika sikukuu yake

                  (b) Herode alisikitika, kwasababu aliona ni atakimbiwa na watu
                 waliokuwa nao katika meza ya chakula na wote waliofika katika
                 sikukuu yake

                  (c) Herode alisikitika, kwasababu aliona ni si haki na ni uonevu  kwa
                 watu waliokuwa nao katika meza ya chakula na wote waliofika katika             
                 sikukuu yake

    (viii) Baada ya kichwa cha Yohana Mbatizaji kukatwa na kukabidhiwa yule kijana alicheza vizuri mbele ya mfalme Herode, ni wapi alikipeleka hicho kichwa?

                  (a) mama yake

                  (b) Kaka yake

                  (c) Rafiki yake
 
MAJIBU

  1. Mbingu za dunia zikamfunukia akaona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake, na sauti kutoka juu ikisema, Huyu ni mwanagu mpendwa wangu, ninayependezwa naye (Mathayo 3:16-17)

  2. Yesu alifunga siku (c) Arobaini (Mathayo 4:1-2)
  3. (i) Yesu alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia, akimsihi akisema, Bwana mtumishi wangu amelala, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana. Yesu akamwambia, (b) Nitakuja, nimponye (Mathayo 8:7)

    (ii) Yule akijibu aksema, Bwana mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu, lakini sema neon na mtumishi wangu atapona. Yesu aliposikia hayo alistajabu akawambia wale waliomfuata (a) Amini na wambie sijaona imani kubwa kama hii kwa yeyote katika Israel (Mathayo 8: 10)

  4. (i) (b) Samaki wawili na mikate mitano .( Mathayo 14:19)

    (ii) (a) kumi na viwili (Mathayo 14:20)

  5. Ni baada ya Yesu kuingia hekaluni na kuona watu wakiuza na kununua, Yesu akapindua meza za wabadili fedha na viti vyao waliokuwa wanauzia njiwa (Mathayo 21:12)
  6.  (i) (b) Yuda alijuta akawarudishia wakuu na makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha. (Mathayo 27:3)

    (ii) (b) Alisema, Nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia (Mathayo 26:43)

    (iii) (a) Alikimbia na kujinyonga. (Mathayo 27:5)

  7. (a) Nazareti 

  8. (a) (i) Mawe yawe mikate

    (ii) Yesu kujitupa chini kutoka katika kinara cha hekalu

    (iii) Kumsujudia Ibilisi (Mathayo 4:4:12)

  9. (a) Bwana ukitaka unaweza kunitakasa (Mathayo 8:2)

  10. (i) (c ) Mfalme Herode (Mathayo 14:2)

    (ii) (a)  Kwasababu alimwambia, Yohana alimwambia sio halali kwa Herode kuwa na nguguye Filipo awe mke wake na Herode. (Mathayo 14:3-4)

    (iii) (b) Kwasababu watu walimuona Yohana Mbatizaji kama Nabii (Mathayo 14:5)

    (iv) (a) Binti Herode (Mathayo 146)

    (v) (a) mama yake (Mathayo 14:8)

    (vi) (c) aliomba kichwa cha Yohana Mbatizaji katika kombe (Mathayo 14:8)

    (vi) (a) Herode alisikitika, kwasababu aliona ni aibu kwa watu waliokuwa nao katika meza ya chakula na wote waliofika katika sikuku yake. (Mathayo 14:9)

    (vii) (a) mama yake (Mathayo 14:11)



    MWISHO
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Mtungaji wa Maswali: Rulea Sanga


CHEMSHA BONGO NA BIBLE 


Inatusaidie wewe na mimi kuijua Biblia na kumpenda Kristo. Nitakuwa nauliza maswali katika kitabu  fulani, kwa mfano mwezi huu wa Julai tutakuwa tunaulizana maswali katika kitabu cha MATHAYO na mwezi unaofuta itakuwa kutoka katika kitabu kingine.

Mwisho wa mwezi kutakuwa na mtihani ambao utaufanya bila ya kuangalia katika Biblia yako. Ninaamini wewe umeokoka kwahiyo hutaweza kunidanganya kwa kuangalizia katika Biblia.

NB: Naomba usiangalie majibu kabla hujajibu kutoka katika akili yako:
SEHEMU YA NANE


MASWALI

1.      Yesu alijibu nini pale alipoulizwa, ni nini dalili ya kuja kwakona ya mwisho ya dunia?

2.      Ni kitu gani Yesu aliwambia wanafunzi wake, baada ya dhiki itakayotokea siku ya mwisho;  kitu gani kitaokea?

3.      Yesu anasema ni nani ajuaye siku ya mwisho?

4.      Kwanini Yesu anatuambia tukeshe?

5.      Kutoka na mfano alioutoa Yesu kuhusia na wale watumwa waliopewa talanta na bwana wao. Wakwanza alipewa talanta taono, wapili akapewa talanta mbili na watatu akapewa talanta moja.

(i) Ni mtumwa yupi alipeleka talanta zaidi baada ya kufanya biashara

(ii) Ni mtumwa yupi alificha talanta na hakurudisha kwa bwana wake.

(iii) Ni kitu gani alimwambia mtumwa wake aliyerudisha talanta zaidi ya zile alizopewa mara ya kwana


MAJIBU
1.      Yesu akajibu akawambia,

(i) Angalieni mtu asiwadanganye, kwa maana wengi watakuja kwa jina langu, wakisema mimi ni kristo; na watadanganya wengi.

(ii) Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi mengi ya vita; angalie msitishwe kwa maana haya hayana budi kutukia, lakini ule mwisho bado

(iii) Taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufame kupigana na ufalme

(iv) Kutakuwa na njaa na matetemeko ya nchi mahali mahali

(v)  Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua, nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwaajili ya jina langu.

(vi) Manabii wengi wa uongo watatokea, na kuwadanganya wengi

(vii) Na kwasababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapotea n.k (Mathayo 24:1-nakuendelea)

2.      Vitu vitakavyotokea baada ya dhiki ni
(i)  Litatiwa giza na mwezi hautatoa mwanga wake na nyota zitaanguka mbinguni

(ii) Nguvu za mbinguni zitatikisika.

(iii) Isaha ya mwana wa Adamu itaonekana mbinguni

(iv) Mataifa yote ya ulimwengu yataoombeleza

(v) Mwana wa Admu ataooneka akija juu ya mawaingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi (Mathayo 24: 29-31)

3.      Yesu asema, walakini habari za siku ile na saa ile hakuna ajuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake. Kwa maana kama ilivyokuwa siku ya Nuhu, ndivyo kutakavyokuwa, kuja kwake Mwana wa Adamu (Mathayo 24:36:41)

4.      Tukeshe kwa maana, hatujui siku ipi atakuja Bwana wetu (Mathayo 24:42)

5.      (i) Ni yule wa kwanza aliyepewa talanta tano 

(ii) Ni yule wa tatu aliyepewa talanta moja

(ii) alimwambia, “Vema mtumwa mwema na mwaminifu kwa machache, nitakuwekea juu ya mengi, ingia katika furaha ya bwana wako
(majibu yote yanapatikana Mathayo 25:14-21)
MWISHO

SEHEMU YA SABA

Hapa blogger wenu, nilikuwa SCOAN kwa Nabii TB Joshua, eneo hili ni la kupatia chakula. Ukichungulia vizuri utaniona upande wa kushoto wa pili. Naomba ujibu maswali vizuri.

MASWALI
  1. Mama yao na Zebedayo alipomwendea Yesu na kutaka wanae wawili wakae mmoja mkuno wa kuume na mwingine mkono wa kushoto katika ufalme wake Yesu.

    (i) Yesu alimjibu nini huyo mama?

    (ii) Yesu alimpomjibu yule mama na kumuuliza, Je, mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi?. Huyo mama alimjibuje?

    (iii) Ni nini Yesu aliwaambia baada ya you mama kumjibu Yesu?
  2. (i) Ni walemavu wa aina gain waliokaa kando ya njia, nao waliposikia Yesu anapita wakapaza sauti, wakisema, Uturehemu, Bwana wa Daudi!?

    (ii) Baada ya Yesu kusikia sauti ya hao walemavu, aliwambia nini?

    (iii) Hao walemavu walipoambiwa na Yesu kitu gani awafanyie, unafikiri aliwajibu nini, na walitatuliwa tatizo lao. Na kama walitauliwa tatizo lao,  Yesu alitumia njia gain kuwaponya ?
  3. Ni baada ya kufanya nini, Yesu aliwaambia, “Imeandikwa, nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala, bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi”.
  4. (i) Kwanini Yesu aliuambia mti unyaeke na yasipatikane matunda milele na baadae mti ukanyauka?

    (ii) wanafunzi wa Yesu baada ya kuona mti umenyauka mara moja, walistajabu sana. Yesu aliwaambia ni wanafunzi kuhusiana na mti huo kunyauka?
  5. Unampenda Yesu? Kama unampenda ni kitu gain utafanya leo kuonyesha unampenda Yesu?


MAJIBU
  1. (i) hamjui mnaloliomba (Mathayo 20:22)

    (ii) twaweza (Mathayo 20:22)

    (iii)  Hakika mtanyea kikombe changu, lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari, na Baba yangu (Mathayo 20:23)
  2. (i) vipofu wawili. (Mathayo 20:30)

    (ii) mnataka niwafanyie nini? (Mathayo 20:32)

    (iii)  walisema, Bwana twataka macho yetu yafumbuliwe. Tatizo lao lilitatuliwa baada ya Yesu kuwagusa macho yao, nao wakamfuata (Mathayo 20:32)
  3. Ni baada ya Yesu kuingia hekaluni na kuona watu wakiuza na kununua, Yesu akapindua meza za wabadili fedha na viti vyao waliokuwa wanauzia njiwa (Mathayo 21:12)
  4. (i) Kwasababu Yesu aliposikia njaa na kuusogelea ule, na mti haukuwa na matunda (Mathayo 21:18)

    (ii) akasema “Amini, nawambia mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya sio hili la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu Ng’oka, ukatupwe baharini, litatendeka. Na yoyote mtakayoomba katika sala mkiamini, mtapokea. (Mathayo 21:21)
      5. Hakuna jibu..jibu uliojibu ni sahihi kwako

MWISHO
SEHEMU YA SITA

MASWALI

  1. (i) Taja jina la mfalme aliyemfunga na kumtia Yohana Mbatizaji gereza?

    (ii) Kwani Yohana alifungwa gerezani?

    (iii) Kwanini mfalme alipoona watu akaogopa kumuua Yohana Mbatiaji?

    (iv) Ni nani aliyecheza mbele ya Herode wakati wa sikuku yake ya kuzaliwa akampendeza Herode kwa uchezaji wake?

    (v) Ni nani alimshauri huyu mtu aliyecheza mbele ya mfalme Herode na mpaka Herode akakubali kutimiza kiapo chake cha kumpa chochote atakachoomba?

    (vi) Huyo aliyemfurahisha Herode kwa kucheza aliomba  nini apewe na huyo mfalme?

    (vii) Unafikiri Herode alifuarahia ilo ombi la huyu aliyecheza vizuri katika sikuku yake ya kuzaliwa? Na kama alifurahi au alisikitika ni kwanini?

    (viii) Baada ya kichwa cha Yohana Mbatizaji kukatwa na kukabidhiwa yule kijana alicheza vizuri mbele ya mfalme Herode, ni wapi alikipeleka hicho kichwa?


  2. (i) Kuna muujiza ambao Yesu aliufanya wa kuiongeza mikate na samaki ambapo wanafunzi wake walikula mpaka wakasaza. Ni mikate mingapi na samaki ngapi ambazo Yesu aliziombea kwa kutazama juu mbinguni kwa Mungu?

    (ii) Masazo yaliyobaki baada ya wanafunzi kula na kushiba ilijaa vikapu vingapi?


  3. Wakati chombo kiahangaika majini kutokana na upepo mbisho au mkali mida ya jioni,

    (i) Yesu alikuwa wapi?

    (ii) Je, alipoona wanafunzi wake wanahangaika na mawimbi bahari kutokana na upepo mkali Yesu alifanya nini?

    (iii) Ni nani aliye alimuomba Yesu aje kwake na apite juu ya maji kama Yesu alivyopita?

    (iv) Unafikiri huyo aliyomba kupita juu ya maji, alifanikiwa hata kidogo kumsogelea Yesu? Elezea kidogo.

    (v) Unafikiri Yesu alipopanda chomboni baharini na wanafunzi wake, upepo alikoma?

    (vi) Ni kitu gani walimwambia Yesu walipokuwa chomboni na hali ya hewa ilipobadilika na kuwa salama?

 MAJIBU
  1. (i) Mfalme Herode (Mathayo 14:2)

    (ii) Kwasababu alimwambia, Yohana alimwambia sio halali kwa Herode kuwa na nguguye Filipo awe mke wake na Herode. (Mathayo 14:3-4)

    (iii) Kwasababu watu walimuona Yohana Mbatizaji kama Nabii (Mathayo 14:5)

    (iv) Binti Herode (Mathayo 146)

    (v) ni mama yake (Mathayo 14:8)

    (vi) aliomba kichwa cha Yohana Mbatizaji katika kombe (Mathayo 14:8)

    (vi) Herode alisikitika, kwasababu aliona ni aibu kwa watu waliokuwa nao katika meza ya chakula na wote waliofika katika sikuku yake. (Mathayo 14:9)

    (vii) alimpelekea mama yake (Mathayo 14:11)


  2. (i) samaki wawili na mikate mitano.( Mathayo 14:19)

    (ii) vikapu kumi na viwili (Mathayo 14:20)


  3. Wakati chombo kinahangaika majini

    (i) Yesu alienda mlimani faragha kuomba (Mathayo 14:23)

    (ii)  Yesu alitembea juu ya bahari huku akiwasogelea wale waliokuwa chomboni baharini na kuwambia “ Jipeni moyo ni mimi msiogope”

    (iii) ni Petro (Mathayo 14:28)

    (iv) Petro alifanikiwa kumsogelea Yesu kwa kupita juu ya maji, lakini alipofika mbele kidogo, upepo ukazidi kuwa mkali na yeye akaanza kuogopa na kuanza kuzama, akapiga kelele aokolewe (Mathayo 14: 20)

    (v) upepo ulikoma (Mathayo 14:32)

    (v) wakamwambia, “Hakika we ni mwana wa Mungu”
    MWISHO

SEHEMU YA TANO
MARUDIO
MASWALI
  1. Malaika alipomtokea Yusufu katika ndoto kuwa aondoke na amchukue mtoto na mamaye waende nchi ya Israel. Je, mfalme Herode alikuwa ameshakufa au mzima?


  2. Malizia mafundisho ya Yesu kwa wanafunzi wake

    (i)  Ninyi ni chumvi ya dunia, lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee?..............................................................................................................

    (ii) Ninyi ni nuru ya……………………………………………………

    (iii)  Msidhani ya kuwa nalikuja kuitugua torati au manabii; la,……………………………………………….

    (iv) Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako
    ana neon juu yako --------------------------------------------------------

    (v) Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, ----------------------------------------------------------

    (vi) Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akikupigaye shavu la kuume,-------------------------------

    (v) Wapendeni adui zenu, waombeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu wa mbinguni,---------------------------------------------------------------------------


  3. Taja majaribu aliyojaribiwa Yesu alipokuwa nyikani


  4. Chagua jibu sahihi

    Baada ya Yesu kumgusa mwenye ukoma kwa mkono wake na kutakasika, Yesu akamwambia

    (a)  Angalia nenda ukawambie na wenzako, na kumuonyesha kuhani wako

    (b) Angalia usimwambie mtu, ila enenda zako ukajionyeshe kwa kuhani ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa iwe ushuhuda wako

    ( c) Angalia nenda na ukamsujudu Mungu wako na kuhani ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa iwe ushuhuda wako


  5. Jibu NDIYO au HAPANA katika maswali yafuatayo:-

    (i) Je, Yohana Mbatizaji alishawahi kufungwa?

    (ii)Yesu alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya aliona ndugu wawili Simoni na Petro na aliwambia, nifuate nami nitawafanya wavuvi wa watu.

    (iii) Yesu alisema, mkiwasamehe watu  makosa yao Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi, bali msipowasamehe watu makosa yenu, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe

    (iv) Yesu anasema tunapofunga tusiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana, kwa maana hujiambia nyuso zao ili wasionekane wamefunga.

    (v) Je, ni kweli Yesu alisema tuyasumbukie ya kesho, kwani hakuna atakayetusumbukia katika suala la kula na kuvaa
MAJIBU
  1. Alikuwa maekufa (Mathayo 2:20)


  2. Mafundisho ya Yesu kwa wanafunzi wake:-

    (i)  Ninyi ni chumvi ya dunia, lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee?, Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu. (Mathayo5:13)

    (ii) Ninyi ni nuru ya ulimwengu (Mathayo5:14)

    (iii)  Msidhani ya kuwa nalikuja kuitugua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza (Mathayo 5:17)

    (iv) Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neon juu yako, iache sadaka yako mbele ya madhabah, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kasha urudi uitoe sadaka yako. (Mathayo 5:23)

    (v) Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, ameshakwisha kuzini naye moyoni mwake (Mathayo 5:27)

    (vi) Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akikupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili (Mathayo 5:39)

    (v) Wapendeni adui zenu, waombeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu wa mbinguni, maana yeye huangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio na haki. (Mathayo 5:43)


  3. Majaribu ya Yesu

    (i) Mawe yawe mikate

    (ii) Yesu kujitupa chini kutoka katika kinara cha hekalu

    (iii) Kumsujudia Ibilisi (Mathayo 4:4:12)


  4. 2.      Baada ya Yesu kumgusa mwenye ukoma kwa mkono wake na kutakasika, Yesu akamwambia, (b) Angalia usimwambie mtu, ila enenda zako ukajionyeshe kwa kuhani ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa iwe ushuhuda wako (Mathayo 8:4)


  5. Majibu yake ni:

     (i) NDIYO (Mathayo 4:12)

    (ii) HAPANA - Yesu alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galila aliona ndugu wawili Simoni aitwaye Petro na Andrea nduguye na aliwambia, nifuate nami nitawafanya wavuvi wa watu  (Mathayo 4:18-20)

    (iii) HAPANA- Anasema tkiwasamehe Baba yetu atatusamehe na tusipowasamehe na Yeye hatatusame (Mathayo 6:14)

    (iv) HAPANA- Ansema tusiwe kama wanafiki ili tuonekane tumefunga (Mathayo 6:16)

    (v) HAPANA-Yesu anasema tusisumbukie ya kesho, kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe, balo tutafute kwanza ufalme wake, na haki yake na hayo yote utazidishiwa.
 MWISHO

SEHEMU YA NNE

Chagu Jibu Sahihi
1.      Yesu aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata. Na tazama akaja mtu mwenye ukoma, akamsujudia akisema,
(a) Bwana ukitaka unaweza kunitakasa
(b) Bwana ukitaka waweza kunibariki
(c) Bwana ukitaka waweza kunihurumia


2.      Baada ya Yesu kumgusa mwenye ukoma kwa mkono wake na kutakasika, Yesu akamwambia
(a)  Angalia nenda ukawambie na wenzako, na kumuonyesha kuhani wako
(b) Angalia usimwambie mtu, ila enenda zako ukajionyeshe kwa kuhani ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa iwe ushuhuda wako
( c) Angalia nenda na ukamsujudu Mungu wako na kuhani ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa iwe ushuhuda wako
3.      (i) Yesu alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia, akimsihi akisema, Bwana mtumishi wangu amelala, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana. Yesu akamwambia,
(a) Amini ameshapona
(b) Nitakuja, nimponye
(c) Nitakuja, nimuokoe na atapona.

(ii) Yule akijibu aksema, Bwana mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu, lakini sema neon na mtumishi wangu atapona. Yesu aliposikia hayo alistajabu akawambia wale waliomfuata
(a) Amini na wambie sijaona imani kubwa kama hii kwa yeyote katika Israel
(b) Amini na wambie sijaona imani kubwa kam hii kwa yeyote katika mkutano huu
(c) Amini na wambie sijaona upendo kubwa kama huu kwa yeyote katika Israel


4.      Baada ya Yesu kuzungukwa na watu wengi kutokana na miujiza aliyoifanya, aliwamuru wanafunzi wake wavuke ng’ambo. Mwanafunzi mmoja akamwambia Bwana, Bwana nipe ruhusa  kwanza niende nikamzike baba yangu. Lakini Yesu akamwambia
(a) Nifuate mimi kama Bwana wako
(b) Nenda ukamzike na unifuate
(c) Nifuate, waache wafu wazike wafu wao
5.      Yesu alipopanda chomboni, akavuka, akafika mjini kwao. Na tazama wakamleta mtu mwenye kupooza, amelala kitandani, naye Yesu alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza,
(a) Jipe moyo mkuu, mwanangu umesamehewa dhambi zako
(b) Mwanangu amini umepona
(c) Jipe moyo mkuu, leo unaenda kupona ugonjwa wako
6.       Ni mtu gani Yesu alikutana naye na kumwambia, nifuate, na yule mtu akamfuata. Lakini alipokaa na kutaka kula naye chakula,  watoza ushuru (Mafarisayo) wakamuliza Yesu , kwanini anakula na mwenye dhambi?
(a) Mathayo
(b) Yuda
(c) Petro


7.      (i) Mjumbe mmoja limwendea Yesu na kusema, Binti yangu saa hivi amekufa, lakini njoo uweke mkono wako juu yake, naye ataishi. Yesu akaondoka na wanafunzi wake mpaka kwa yule mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka…………………alikuja kwa nyuma , akagusa pindo la vazi lake.
(a) kumi na tatu
(b) kumi na mbili
(c) kumi na moja

(ii) Baada ya kuguswa vazi la pindo lake, Yesu akageuka akamwambia
(a) Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya.
(b) Umepona, ondoka ukashuhudie.
(c) Kuwa na imani utapona
MAJIBU
1.      Yesu aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata. Na tazama akaja mtu mwenye ukoma, akamsujudia akisema, (a) Bwana ukitaka unaweza kunitakasa (Mathayo 8:2)

2.      Baada ya Yesu kumgusa mwenye ukoma kwa mkono wake na kutakasika, Yesu akamwambia, (b) Angalia usimwambie mtu, ila enenda zako ukajionyeshe kwa kuhani ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa iwe ushuhuda wako (Mathayo 8:4)


3.      (i) Yesu alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia, akimsihi akisema, Bwana mtumishi wangu amelala, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana. Yesu akamwambia, (b) Nitakuja, nimponye (Mathayo 8:7)

(ii) Yule akijibu aksema, Bwana mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu, lakini sema neon na mtumishi wangu atapona. Yesu aliposikia hayo alistajabu akawambia wale waliomfuata (a) Amini na wambie sijaona imani kubwa kama hii kwa yeyote katika Israel (Mathayo 8: 10)


4.      Baada ya Yesu kuzungukwa na watu wengi kutokana na miujiza aliyoifanya, aliwamuru wanafunzi wake wavuke ng’ambo. Mwanafunzi mmoja akamwambia Bwana, Bwana nipe ruhusa  kwanza niende nikamzike baba yangu. Lakini Yesu akamwambia, (c) Nifuate, waache wafu wazike wafu wao


5.      Yesu alipopanda chomboni, akavuka, akafika mjini kwao. Na tazama wakamleta mtu mwenye kupooza, amelala kitandani, naye Yesu alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, (a) Jipe moyo mkuu, mwanangu umesamehewa dhambi zako (Mathayo9:2)


6.      (a) Mathayo (Mathayo 9:9)
7. (i) Mjumbe mmoja limwendea Yesu na kusema, Binti yangu saa hivi amekufa, lakini njoo uweke mkono wako juu yake, naye ataishi. Yesu akaondoka na wanafunzi wake mpaka kwa yule mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka (b) kumi na mbili  alikuja kwa nyuma , akagusa pindo la vazi lake. (Mathayo 9:20)

  (ii) Baada ya kuguswa vazi la pindo lake, Yesu akageuka akamwambia,
       (a) Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. (Mathayo 9:22)


MWISHO

SEHEMU YA TATU


MASWALI
Chagua jibu sahihi
  1. Yesu alipopandishwa na Roho nyikani ili ajaribiwe na ibilisi, alifunga kula siku ngapi?
    (a) 10 (b) 45 (c) 40
  2. Taja majaribu aliyojaribiwa Yesu alipokuwa nyikani
  3. Kutokana na majaribu aliyojaribiwa Yesu na Ibilisi, alimjibu nini pale alipoambiwa

    (i) Ageuze mawe kuwa mkate

    (ii) Yesu kujitupa chini kutoka katika kinara cha hekalu

    (iii) Kumsujudia Ibilisi
  4. Ni majaribu mangapi Yesu alijaribiwa na Ibilisi nyikani?
  5. Jibu NDIYO au HAPANA katika maswali yafuatayo:-

    (i) Je, Yohana Mbatizaji alishawahi kufungwa?

    (ii)Yesu alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya aliona ndugu wawili Simoni na Petro na aliwambia, nifuate nami nitawafanya wavuvi wa watu.

    (iii) Yesu alisema, mkiwasamehe watu  makosa yao Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi, bali msipowasamehe watu makosa yenu, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe

    (iv) Yesu anasema tunapofunga tusiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana, kwa maana hujiambia nyuso zao ili wasionekane wamefunga.

    (v) Je, ni kweli Yesu alisema tuyasumbukie ya kesho, kwani hakuna atakayetusumbukia katika suala la kula na kuvaa
  6. Malizia mafundisho ya Yesu kwa wanafunzi wake

    (i)  Ninyi ni chumvi ya dunia, lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee?..............................................................................................................

    (ii) Ninyi ni nuru ya……………………………………………………

    (iii)  Msidhani ya kuwa nalikuja kuitugua torati au manabii; la,……………………………………………….

    (iv) Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako
    ana neon juu yako --------------------------------------------------------

    (v) Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, ----------------------------------------------------------

    (vi) Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akikupigaye shavu la kuume,-------------------------------

    (v) Wapendeni adui zenu, waombeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu wa mbinguni,---------------------------------------------------------------------------
  7. Jaza nafasi zilizoachwa wazi ili kukamilisha ujumbe wa Yesu kwa wanafunzi wake

    (i)  Angalia msifanye wema machoni pa watu, ---------------------------; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa…………………….yenu wa mbinguni.

    (ii) Basi wewe utoapo sadaka usipige panda mbele yako, kama --------------------------- wafanyavyo katika masinagogi na njiani ili --------------------------na watu.

    (iii) Tena msalipo msiwe kama ------------------, kwa maana wao wanapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia ili……………………na watu.



MAJIBU
  1. Yesu alifunga siku (C ) 40(Mathayo 4:1-2)
  2. Majaribu ya Yesu

    (i) Mawe yawe mikate

    (ii) Yesu kujitupa chini kutoka katika kinara cha hekalu

    (iii) Kumsujudia Ibilisi (Mathayo 4:4:12)
  3. Yesu alisema:

    (i) Mtu hataishi kwa mkate tu ila kwa kila Neno litokalo katika kinywa cha Mungu (Mathayo 4:4)

    (ii) Usimjaribu BWANA Mungu wako (Mathayo 4:7)

    (iii) Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye pekee yake (Mathayo 4:10)
  4. Majaribu yalikuwa matatu (Mathayo 4:4-12)
  5. Majibu yake ni:

     (i) NDIYO (Mathayo 4:12)

    (ii) HAPANA - Yesu alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galila aliona ndugu wawili Simoni aitwaye Petro na Andrea nduguye na aliwambia, nifuate nami nitawafanya wavuvi wa watu  (Mathayo 4:18-20)

    (iii) HAPANA- Anasema tkiwasamehe Baba yetu atatusamehe na tusipowasamehe na Yeye hatatusame (Mathayo 6:14)

    (iv) HAPANA- Ansema tusiwe kama wanafiki ili tuonekane tumefunga (Mathayo 6:16)

    (v) HAPANA-Yesu anasema tusisumbukie ya kesho, kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe, balo tutafute kwanza ufalme wake, na haki yake na hayo yote utazidishiwa.
  6. Mafundisho ya Yesu kwa wanafunzi wake:-

    (i)  Ninyi ni chumvi ya dunia, lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee?, Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu. (Mathayo5:13)

    (ii) Ninyi ni nuru ya ulimwengu (Mathayo5:14)

    (iii)  Msidhani ya kuwa nalikuja kuitugua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza (Mathayo 5:17)

    (iv) Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neon juu yako, iache sadaka yako mbele ya madhabah, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kasha urudi uitoe sadaka yako. (Mathayo 5:23)

    (v) Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, ameshakwisha kuzini naye moyoni mwake (Mathayo 5:27)

    (vi) Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akikupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili (Mathayo 5:39)

    (v) Wapendeni adui zenu, waombeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu wa mbinguni, maana yeye huangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio na haki. (Mathayo 5:43)
  7. Ujumbe wa Yesu kwa wanafunzi wake

    (i)  Angalia msifanye wema machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu wa mbinguni. (Mathayo 6:1)

    (ii) Basi wewe utoapo sadaka usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani ili watukuzwe na watu. (Mathayo 6:2)

    (iii) Tena msalipo msiwe kama wanafiki, kwa maana wao wanapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia ili waonekanae na watu
MWISHO

SEHENU YA KWANZA

MASWALI
  1. Yesu Kristo alizaliwa wapi?
  2. Kwanini mfalme Herode aliwambia mamajuzi waende wakaulizie mambo ya mtoto Yesu Bethelehem
  3. Zawadi gani mamajuzi walimtolea Yesu baada ya kumuona amezaliwa Bethelehem?
  4. Unafikiri kwanini Yusufu aliambiwa na malaika aondoke na mtoto Yesu na akimbie naye Misri?
  5. Watoto waliokuwa wanaamri kuuawa na mfalme Herode ni umri gan? 
  6. Malaika alipomtokea Yusufu katika ndoto kuwa aondoke na amchukue mtoto na mamaye waende nchi ya Israel. Je, mfalme Herode alikuwa ameshakufa au mzima?
  7. Baada ya kusikia kuwa Herode amekufa Misri, Yusufu, Yesu na Bikira Maria  walitoka Israel ni wapi walienda kuishi?
  8. Ni nyika zipi Yohana mbatizaji alikuwa anahubiri? Na ni maneno gain alikuwa anasema?
  9. Vazi gain Yohana alikuwa amelivaa wakati anahubiri habari njema?
  10. Chakula gain Yohana mbatizaji alikuwa anakula?
  11. Mto gani Yohana Mbatizaji alitumia kuwabatiza watu huku akiwaungamisha dhambi zao?
  12. Ubatizo gani Yohana alikuwa anabatiza watu na alitumia nini kubatiza?  Yesu alibatiza ubatizo wa aina gani na alitumia nini kubatiza?
  13.  Ni nani alimbatiza Yesu na ni wapi alimbatiza?
  14. Unafikri kwanini Yohana alitaka kukataa kumbatiza Yesu?
  15. Kitu gani kilitokea baada ya Yesu kubatizwa? 
MAJIBU
1.      Bethelehemu ya Uyahudi (Mathayo 2:1)
2.      Herode naye alitaka amsujudie (Mathayo 2:8)
3.      Walimtolea  tunu, dhahabu na utunu wa manemane (Mathayo 2:11)
4.      Kwasababu Herode alitaka kumwangamiza Yesu (Mathayo 2:13)
5.      Umri wa miaka miwili na wale waliopungua miaka hiyo (Mathayo 2:16)
6.      Alikuwa maekufa (Mathayo 2:20)
7.      Waliishi Nazareti  mathayo 2:23)
8.      Alihubiri katika nyika ya Uyahudi na alikuwa anahubiri watu kutubu kwa maana ufalme wa Mungu umekaribia (Mathayo 3:1-2)
9.      Alivaa vazi la Singa za ngamia, na mshipi wa ngozi ya kunoni.
10.  Alikuwa anakula nzige na asali ya mwitu (Mathayo 3: 4)
11.   Mto Yordani (Mathayo 3:5)
12.   Yohana alibatisa ubatizo wa toba kwa njia ya maji wakati Yesu alibatiza kwa njia ya Roho Mtakatifu na moto (Mathayo 3:11)
13.  Aliye mbatiza Yesu ni Yohana katika mto Yordan (Mathayo 3:13)
14.  Yohana alitaka kubatizwa na Yesu kwasababu alijua ana nguvu kuliko yeye (Mathayo 3:14)
15.  Mbingu za dunia zikamfunukia akaona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake, na sauti kutoka juu ikisema, Huyu ni mwanagu mpendwa wangu, ninayependezwa naye (Mathayo 3:16-17)



Comments